Header Ads

WATOTO YATIMA WAPATIWA MSAADA

Jinsi wanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa wanaosoma shahada ya sheria mwaka wa tatu waliadhimisha uhuru wa habari kwa kuwatembelea watoto yatima wenye shida katika kituo cha Teresia Sister kilichoko Tosamaganga na kuwakabidhi msaada mbalimbali yenye thamani ya shilingi milioni 1na kucheza nao (picha zote na Denis Mlowe)
=======  ========
Na Denis Mlowe,Iringa

KITUO cha kulelea watoto yatima na wenye shida cha Teresia Sister kilichoko Tosamanga mkoani Iringa kimepatiwa msaada wa vitu mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni 1 na wanafunzi wa mwaka wa tatu wanaochukua shahada ya sheria kutoka chuo kikuu cha Iringa(Tumaini)
 
Akikabidhi misaada hiyo mkufunzi wa sheria wa chuo hicho Penina Manyanki akiambatana na wanafunzi hao,alisema kuwa wamehamua kutoa misaada hiyo kwa watoto hao wenye mahitaji kutokana na kusahalika katika jamii na kwamba misaada hiyo itawasaidia  kuwafanya wafurahi na kutambua jamii ipo pamoja nao.
 
Alisema imekuwa kasumba kwa watu wengi kuwasahau watoto yatima na wanaohitaji msaada hivyo waliamua kuchangishana wanafunzi wa mwaka wa tatu na kuwapeleka misaada hiyo kwa watoto hao wenye umri wa miezi miwili hadi miaka sita wanaolelewa katika kituo hicho.

“Huu ni mwanzo tu wa kuwasaidia watoto hawa na naomba sana jamii iweze kuwasaidia watoto hawa misaada mbalimbali watambue kuwa kuna watu wako nyuma yao na wanawapenda sana na kama unavyoona watoto wamefurahi sana kuungana na dada na kaka zao “ alisema Manyanki
 
Aidha Manyanki aliyataka mashirika na watu binafsi kujitokeza kutoa misaada kwa watoto hao ili kujengea imani ya kutoona kama wanatengwa katika jamii inayowazunguka
 
Manyanki alivitaja vitu vilivyotolewa kuwa ni pamoja na Sukari,Mchele,Mafuta ya Kula,Sabuni ya kufulia,unga wa ngano,juisi na maharage kwa ajili ya kuwasaidia watoto hao.
 
Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa kituo Sister Mlezi wa Kituo hicho Sr. Hellen Kihwele aliwashukuru wanafunzi hao kwa misaada kama hiyo ambayo imekuwa ikisadia watoto kujikimu katika mahitaji yao ya kila siku.
 
Sister Hellen alitaja changamoto zinazowakabili kuwa ni pamoja na ukosefu wa chakula,madawa,mavazi ambapo aliomba serikali kusaidia kutatua kero hizo ikiwa ni pamoja na kuwajenga watoto mazingira mazuri ya kuishi.

Alitoa wito kwa wanawake kuacha tabia ya kuwatupa watoto wasio kuwa na hatia na kuisababishia jamii malezi ingali wazazi wao wapo na wanaendelea kuponda raha.

No comments:

Powered by Blogger.