Skuli ya Kitope yapatiwa msaada wa madeski na NMB
Baadhi ya Wanafunzi wa Skuli ya Kitope
waliohudhuria hafla ya kupatiwa vikalio vya skuli za Donge na Kitope
iliyofanyika katika Skuli ya Sekondari ya Kitope.
Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif
Ali Iddi akipokea Madeski 50 kwa ajili ya skuli ya Sekondari ya Kitope
kutoka kwa Meneja wa Tawi la Benki ya NMB Bwana Bakari Khamis Mohd.
kwa Meneja wa Tawi la Benki ya NMB
Bwana Bakari Khamis Mohd akimkabidhi madeski 50 Mbunge wa Jimbo la Donge
Mh. Sadifa Juma Khamis kwa ajili ya Skuli ya Sekondario ya Doonge.
Balozi Seif akiwa katika picha ya
pamoja na Uongozi wa Benki ya NMB mara baada ya hafla ya makabidhiano ya
madeski kwa ajili ya skuli za Donge na Kitope.
Kushoto ya Balozi ni Mbunge wa Jimbo la Donge Mh. Sadifa Juma mKhamis na Mke wa Balozi Seif Mama Asha Suleiman Iddi.
Kulia
ya Balozi ni Meneja wa NMB Tawi la Zanzibar Bwana Bakari Khamis Moha na
Mwenyekiti wa Skuli ya Kitope Sekondari Nd. Ali Mussa.
Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.
Na Othman Khamis Ame, OMPR
Benki
ya kuhudumia Wananchi wa Kawaida Nchini { NMB } imekabidhi mchango wa
Vikalio 100 kwa ajili ya kusaidia sekta ya Elimu katika Skuli za
Sekondari za Donge na Kitope zilizomo ndani ya Wilaya ya Kasakazini “ B “
Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Msaada
huo wa Vikalio wenye gharama ya shilingi za Kitanzania Milioni Kumi
utasaidia kupunguza uhaba wa madeski kwa Skuli hizo za Donge na Kitope
ambapo kila Skuli imefanikiwa kupata madeski 50.
Meneja
wa Tawi la NBC Zanzibar Bwana Bakari Khamis Moh’d alikabidhi msaada huo
kwa Mbunge wa Jimbo la Kitope Balozi Seif Ali Iddi pamoja na Mbunge wa
Jimbo la Donge Mh. Sadifa Juma Khamis hafla iliyofanyika hapo katika
skuli ya Sekondari Kitope.
Meneja
huyo wa Tawi la Benki ya NMB Bwana Bakari aliiomba Jamii kuendelea
kuiunga mkono Benki hiyo ili kusaidia kuipa nguvu za kiutendaji
itakaoongeza kasi ya kusaidia harakati za Kijamii Nchini.




No comments:
Post a Comment