Header Ads

SERIKALI YA UJERUMANI KUTUMIA EURO MILIONI 10 KUKARABATI RELI YA KATI


DSC_0072
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Dkt. Frank Steinmeier akizungumza waandishi wa habari kwenye mkutano huo jijini Dar es Salaam na kuelezea mafanikio ya ushirikiano wa nchi hizo mbili.

Membe alilisisitiza kwamba ziara ya Waziri mpya wa mambo ya nje kutoka Ujerumani ina manufaa makubwa kwa Tanzania kwa sababu amekuja na wawekezaji 65 kutoka maeneo mbalimbali.

Amesema kuwa ukarabati wa reli ya kati ni muhimu katika kudumisha ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kati ya nchi hizo mbili kwa maslahi ya watu wao. “reli ya kati kama mnavyojua ilijengwa na Wajerumani mwaka 1913 na kwa sasa ina miaka karibu mia moja na kitu,” aliongeza Waziri Membe.

Kwa upande wake, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani, Dkt. Steinmeier amesema kuwa nchi yake itaendelea kudumisha ushirikiano wa kiuchumi na kijamii na Tanzania katika jitihada za kuharakisha maendeleo ya nchi na watu wake. Amesema kuwa serikali ya Ujerumani imeamua kukarabati reli ya kati katika jitihada za kukumbuka na kudumisha historia ya muda mrefu kati ya nchi hizo mbili. “najisikia furaha na faraja kuona nchi yaTanzania inapiga hatua mbele kimaendeleo baada ya uhuru wake,” amesema
DSC_0096
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mh. Bernard Membe akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ushirikiano wa kihistoria na kiuchumi kati ya Tanzania na Ujerumani jijini Dar es Salaam.
DSC_0112
Baadhi ya wageni waalikwa na maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ubalozi wa Ujerumani nchini.
DSC_0043
Sehemu ya waandishi wa habari nchini pamoja na waandishi kutoka nje ya nchi waliohudhuria mkutano huo leo jijini Dar.
DSC_0116
Mwandishi wa gazeti la Tanzania Daima akiuliza swali wakati wa mkutano huo.

No comments:

Powered by Blogger.