SAMSUNG TANZANIA YAENDELEA KUTOA ZAWADI KWA WASHINDI WALIONUNUA BIDHAA HALISI ZA SAMSUNG TANZANIA
Mhasibu Mkuu wa Kampuni ya Samsung
Tanzania, Bw Ibrahim Kombo akiongea na waandishi wa habari (hawapo
pichani) wakati wa Zoezi la kukabidhi zawadi kwa washindi wa
kinyanganyiro cha Promosheni ya E-warranty inayoendeshwa na Kampuni ya
Samsung Tanzania, Mteja anayenunua Bidhaa yoyote kutoka Samsung Tanzania
atajisajili katika mfumo wa E-warrant ambapo itachezeshwa bahati nasibu
na washindi kupatikana.
Mhasibu Mkuu wa Kampuni ya Samsung
Tanzania (Kulia) akimkabidhi zawadi ya Microwave, Ndugu Joseph Gobson
Nswila mara baada ya kuchaguliwa kuwa mmoja wa mshindi wa promosheni ya
E-warrant inayoendeshwa na Kampuni ya Samsung Tanzania
Mshindi wa zawadi ya Home Theater
kutoka Samsung Tanzania, Bw John Macharia akipokea zawadi yake kutoka
kwa Mhasibu wa Samsung Tanzania, Bw Ibrahim Kombo wakati wa makabidhiano
ya zawadi kwa washindi wa promosheni ya E-warranty, Makabidhiano hayo
yamefanyika katika Duka la Samsung lililopo Katika Jengo la Quality
Center, barabara ya Nyerere Road.
Baba Mzazi wa Lugano Msokwa, ambae
amemwakilisha mwanae, Lugano Msokwa ambae amejishindia zawadi ya Simu
aina ya Samsung Galaxy Tab 10.1 kutoka Samsung baada ya kununua simu
halisi na kuingia kwenye bahati nasibu.
Mshindi Wa Runinga kutoka Samsung
Tanzania, Bw Khalil Sherali akipokea zawadi yake ya Runinga kutoka kwa
Mhasibu mkuu wa Samsung Tanzania, Bw Ibrahim Kombo wakati wa
makabidhiano ya zawadi za washindi wa promosheni ya E-warrant kutoka
Samsung Tanzania yaliyofanyika katika Duka la Samsung lililopo Katika
Jengo la Quality Center, lililopo Katika Barabara ya Nyerere, Jijini Dar
Es Salaam.
Washindi wa Promosheni ya
E-warrant inayoendeshwa na Kampuni ya Samsung Tanzania wakiwa katika
picha ya Pamoja mara baada ya kumalizika kwa zoezi la kukabidhi zawadi
hizo.
Mmoja
wa Washindi wa Runinga Kutoka Samsung Tanzania, Bw Khalil Sherali
akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) mara baada ya
kukabidhiwa zawadi yake ya Runinga kutoka Samsung Tanzania
No comments:
Post a Comment