Header Ads

POLISI YAJIPANGA VIZURI KUZUIA VURUGU SIKU YA UCHAGUZI KALENGA


Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa Ramadhani A. Mungi akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao Makuu ya Jeshi la Polisi mkoa wa Iringa na kuwambia namna Jeshi hilo lilivyojipanga kulinda amani na kuwasihi wananchi wote wa Kalenga kujitokeza na kwenda kupiga kura kwa Amani.
Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi mkoani Iringa  Ramadhani A. Mungi akizungumza na waandishi wa habari na kuwaeleza namna walivyojipanga kulinda amani siku ya uchaguzi Kalenga na kuhakikishia wananchi wa Kalenga kuwa jeshi la Polisi limejipanga kupambana na wahalifu ,leo tarehe 14 Machi 2014.

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
“PRESS RELEASE”
 
 Ndugu waandishi wa habari , kwa niaba ya askari Polisi wa Mkoa wa Iringa, nitumie fursa hii kuwakaribisha hapa ofisini kwetu.
 
Ndugu zangu tumeitana hapa asubuhi hii ili niweze kuwapa taarifa ya usalama katika Mkoa wetu wa Iringa hususani katika Jimbo la Kalenga katika kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi wa Jimbo la Kalenga na usalama wa siku ya uchaguzi wenyewe.Ili iwe rahisi kueleweka taarifa hii nitaitoa kwa kifupi sana kwa kuigawa katika maeneo matatu. Eneo la kwanza ni juu ya wapi tunataka tupafikie  ( Where we want to go ), eneo la pili ni lile la wapi tulipo ( Where are we? ) na eneo la tatu ni jinsi gani tutafika huko ( How do we get there ). Tuanze na wapi   tunataka   tupafikie. Sisi  Polisi Mkoa  wa  Iringa tunataka  wananchi  wa  Kalenga  wapige kura  kwa  amani na  utulivu  mkubwa siku  ya   jumapili tarehe  16/3/2014. Hii   ndio  dira yetu  na  tutahakikisha tunafika  hapo. 

No comments:

Powered by Blogger.