POLISI YAJIPANGA VIZURI KUZUIA VURUGU SIKU YA UCHAGUZI KALENGA

Kamishna
Msaidizi wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa Ramadhani A. Mungi
akizungumza na waandishi wa habari kwenye makao Makuu ya Jeshi la Polisi
mkoa wa Iringa na kuwambia namna Jeshi hilo lilivyojipanga kulinda
amani na kuwasihi wananchi wote wa Kalenga kujitokeza na kwenda kupiga
kura kwa Amani.

Kamishna
Msaidizi wa Jeshi la Polisi mkoani Iringa Ramadhani A. Mungi
akizungumza na waandishi wa habari na kuwaeleza namna walivyojipanga
kulinda amani siku ya uchaguzi Kalenga na kuhakikishia wananchi wa
Kalenga kuwa jeshi la Polisi limejipanga kupambana na wahalifu ,leo
tarehe 14 Machi 2014.
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI
JESHI LA POLISI TANZANIA
“PRESS RELEASE”
Ndugu waandishi wa habari , kwa niaba ya askari Polisi wa Mkoa wa Iringa, nitumie fursa hii kuwakaribisha hapa ofisini kwetu.
Ndugu
zangu tumeitana hapa asubuhi hii ili niweze kuwapa taarifa ya usalama
katika Mkoa wetu wa Iringa hususani katika Jimbo la Kalenga katika
kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi wa Jimbo la Kalenga na usalama wa
siku ya uchaguzi wenyewe.Ili iwe rahisi kueleweka taarifa hii nitaitoa
kwa kifupi sana kwa kuigawa katika maeneo matatu. Eneo la kwanza ni juu
ya wapi tunataka tupafikie (
Where we want to go ), eneo la pili ni lile la wapi tulipo ( Where are
we? ) na eneo la tatu ni jinsi gani tutafika huko ( How do we get there
). Tuanze na wapi tunataka tupafikie. Sisi Polisi Mkoa wa Iringa tunataka wananchi wa Kalenga wapige kura kwa amani na utulivu mkubwa siku ya jumapili tarehe 16/3/2014. Hii ndio dira yetu na tutahakikisha tunafika hapo.
No comments:
Post a Comment