Header Ads

PICHA ZA MOJA KWA MOJA KUTOKA CHALINZE:HEBU JIONEE MAANDALIZI YA UZINDUZI WA KAMPENI CCM CHALINZE YALIVYOANZA VIZURI


Maandalizi ya mkutano mkubwa wa uzinduzi wa kampeni za Ubunge kupitia CCM jimbo la Chalinze yaendelea vizuri ambapo jioni ya leo Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana anatarajiwa kuhutubia wakazi wa Chalinze na Vitongoji vyake pamoja na kumnadi mgombea wa ubunge kupitia CCM Ndugu Ridhwani Kikwete.
 Barabara Kuu iendayo mikoa ya Tanga,Kilimanjaro na Arusha ikiwa imependeza kwa bendera za CCM ,ambapo masaa machache yajayo kutakuwa na mkutano mkubwa wa hadhara wa uzinduzi wa kampeni za ubunge CCM.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi ambaye pia ni mratibu wa Kampeni za Ubunge Jimbo la Chalinze akisoma vichwa vya habari vya magazeti ya leo kwenye moja ya vibanda vya magazeti Chalinze huku sehemu kubwa ya maeneo yote yakiwa yamebandikwa mabango yenye picha za mgombea kiti cha ubunge kupitia CCM Ndugu Ridhwani Kikwete.
 Mratibu wa Kampeni za Ubunge CCM jimbo la Chalinze Nape Nnauye akibadilisha na Kamanda waVijana mkoa wa pwani wakati wa kukagua hatua za mwisho za maandalizi ya mkutano wa ufunguzi wa Kampeni.

No comments:

Powered by Blogger.