Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema amesema baadhi ya mawaziri wamekuwa wakaidi kufuata ushauri wa kisheria ambao amekuwa akiutoa na kwamba hicho ndicho chanzo cha matatizo yote yanayotokea katika utendaji wa Serikali, yakiwamo yale yaliyobainika katika Ripoti ya Operesheni Tokomeza Ujangili.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema.
---
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema amesema
baadhi ya mawaziri wamekuwa wakaidi kufuata ushauri wa kisheria ambao
amekuwa akiutoa na kwamba hicho ndicho chanzo cha matatizo yote
yanayotokea katika utendaji wa Serikali, yakiwamo yale yaliyobainika
katika Ripoti ya Operesheni Tokomeza Ujangili.
Wakati Jaji Werema akiwananga mawaziri, kwa upande
mwingine amemsifia Rais Jakaya Kikwete akisema kuwa yeye si kama
mawaziri wake kwani ni msikivu na anayeshaurika. Akizungumza na
mwandishi wetu jana, Jaji Werema alisema endapo ushauri ambao amekuwa
akiutoa mara kadhaa kwa mawaziri ungezingatiwa, kilichotokea bungeni
mwishoni mwa wiki cha mawaziri kung’oka kisingekuwapo.
“Tunatakiwa kuiga msemo wa Mkuu wa Jeshi la
Polisi, Said Mwema kuwa ‘tii sheria bila shuruti’, Rais tunamshauri na
anashaurika kwa nini mawaziri wakatae kuzingatia ushauri?” alisema
Werema na kuongeza:
“Mawaziri hawatakiwi kujifanyia tu mambo yao. Tunawaandikia barua lakini zinakwenda na yanafanyika yaleyale... Hata mimi nikionekana kukiuka sheria na kanuni naweza kuwajibishwa kwa kuwa hakuna aliye juu ya sheria.”Kwa habari zaidi Bofya na Endelea.........
“Mawaziri hawatakiwi kujifanyia tu mambo yao. Tunawaandikia barua lakini zinakwenda na yanafanyika yaleyale... Hata mimi nikionekana kukiuka sheria na kanuni naweza kuwajibishwa kwa kuwa hakuna aliye juu ya sheria.”Kwa habari zaidi Bofya na Endelea.........
No comments:
Post a Comment