Rais Kikwete azindua Ukumbi wa Mpya wa Bunge la Afrika Mashariki jijini Arusha
Spika wa Bunge la Tanzania Mhe.
Anne Makinda akimpokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.
Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipokuwa akiwasili katika jengo jipya la
Jumuiya ya Afrika Mashariki Jijini Arusha kwa lengo la kuzindua Ukumbi
wa Bunge la Afrika Mashariki ulioko katika jengo hilo.
Spika wa Bunge la Africa Mashariki
Mhe. Margret Natongo Zziwa (kulia) akimkaribisha Spika wa Bunge la
Tanzania Mhe. Anne Makinda katika jengo hilo.
Spika wa Bunge Afrika
Mashariki,Mhe. Margret Natongo Zziwa akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania,Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) ili
kulihutubia Bunge la Afrika Mashariki.Kulia ni Spika wa Bunge la
Tanzania Mhe. Anne Makinda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akilihutubia Bunge la Afrika
Mashariki wakati alipofika kuzindua Ukumbi Mpya wa Bunge la Afrika Mashariki ulioko katika jengo jipya la Jumuiya ya Afrika Mashariki Jijini Arusha.
Baadhi ya Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki wakiwa katika picha ya pamoja na Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete.
Jengo jipya la Jumuiya ya Afrika Mashariki.Picha na Prosper Minja- Bunge.
No comments:
Post a Comment