Mkuu
wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama akisoma hotuba ya kushukuru
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kwa msaada wa mgodoro 200 na vyandarua 200
vyenye thamani ya Sh. mil. 15 katika hafla iliyofanyika mwanzoni mwa
wiki, mjini Moshi. Hospitali ya Kilema itapata msaada wa magodoro 100 na
vyandarua 100 na Hospitali ya Wilaya ya Hai itapata magodoro 100 na
vyandaruwa 100.
Mkuu
wa Mkoa wa Kilimanjaro, Leonidas Gama (wa tatu kushoto) akikabidhi
moja kati ya magodoro 100 na vyandarua 100 kwa Mganga Mkuu wa Hospitali
ya Kilema iliyopo Moshi vijijini, Dk. Wonanji Timoth msaada uliotolewa
kwa hospitali hiyo na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL),katika hafla
iliyofanyika mwanzoni mwa wiki.Tbl ilitoa pia msaada kama huo kwa
Hospitali ya Wilaya ya Hai. Kushoto ni Mkurugenzi wa Uhusiano na Sheria
wa TBL, Steven Kilindo.
Mkurugenzi
wa Mawasiliano na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Stephen
Kilindo (kushoto) akimkabidhi godoro Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,
Leonidas Gama ikiwa ni sehemu ya msaada wa magodoro 200 na vyandarua 200
vyenye thamani ya sh. mil. 15 vitakavyogawiwa kwa Hospitali za Kilema
na Hai mkoani humo. Hafla hiyo ilifanyika hivi karibuni mjini Moshi.
Baadhi ya wauguzi wa Hospitali hiyo, wakishuhudia makabidhiano hayo.
Reviewed by
crispaseve
on
7:04 AM
Rating:
5
No comments:
Post a Comment