Header Ads

NHC yanyang’anya mashine za kufyatulia matofari baada ya Halmashauri za Mikoa baada ya kushindwa kutumia fursa hiyo

● Mkoa wa Katavi na Rukwa washindwa kutumia fursa ya msaada huo ● NHC yanyang’anya mashine Halmashauri za Mikoa hiyo ● Zatakiwa kuomba upya mashine hizo na kuunda vikundi imara Katika kuhakikisha kuwa rasilimali za umma zinatunzwa, kutumika ipasavyo na kuhakikiwa, NHC imeendelea kuwakagua vijana waliopewa msaada wa mashine za kufyatulia matofali yatakayowezesha wananchi kujijengea nyumba za gharama nafuu katika Halmashauri zote za Mikoa ya Katavi, Mbeya na kukamilika Mkoani Iringa. 

Kwa ujumla, vijana wana ari ya kutosha ingawa wana changamoto zinazohitaji msukumo wa Halmashauri zao, hasa za masoko ya matofali yao pamoja na mtaji wa kuwawezesha kuendelea na uzalishaji wa benki ya matofali ya kuuzia wananchi. Katika ziara ya NHC Wakurugenzi Watendaji wa Wilaya hizo wameomba NHC isiwanyang’anye mashine na wameahidi kuwapa vijana mikopo na kuwasaidia malighafi za kuwawezesha kutengezea matofali hayo ikiwemo mchanga, sementi na udongo maalum kwa kazi hiyo. 

Hata hivyo, Mikoa ya Rukwa na Katavi muitikio wa vijana na Halmashauri hizo ukiacha Halmashauri ya Mlele ambayo inafanya vizuri, umekuwa hafifu sana na Shirika limelazimika kuzinyang’anya Halmashauri hizo mashine na kuzitaka kuomba upya kama bado wana azma ya kutumia mashine hizo kujiletea maendeleo ya kuwa na nyumba bora na kukuza ajira kwa vijana wao. Fuatilia yaliyojiri katika uhakiki huo katika picha.
New Picture (1)  
Kikundi cha ‘Mshikamano’ katika Halmashauri ya Wilaya ya Ileje kikimsikiliza Meneja wa Huduma kwa Jamii wa NHC BW. Muungano Saguya akiwaelezea namna ya kukuza ujuzi na kutumia Halmashauri zao kuongeza ufanisi wa kazi alipowatembelea nakusaidia kuondoa changamoto zinazowakabili. Vijana hao wameshapewe eneo la muda la kuendesheea shughuli zao na wameanza kutengeneza tofali kwa ajili ya kuwauzia wanmanchi.
New Picture (2)
Hii ndiyo hali iliyojitokeza Mkoani Katavi katika Halmashauri ya Mji wa Mpanda pale NHC ilipolazimika kuzitwaa mashine ilizotoa msaada kwa vijana ili waweze kujiajiri. Kikundi hiki cha Mpanda Hotel ni mojawapo ya vikundi vilivyonyang’anywa mashine Mkoani Katavi na Rukwa kwa Halmashauri sita za Mikoa hiyo ukiacha Mlele inayofanya vizuri, kushindwa kuzitumia mashine hizo ipasavyo. Halmashauri hizo zimetakiwa kuomba upya mashine hizo na kuunda vikundi imara baada ya kubainika kuwa vikundi vya awali vilundwa kisiiasa.
New Picture (3)
Kikundi cha vijana cha ITIMBA kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Vijijini kikimsikiliza` Meneja wa Huduma kwa Jamii wa NHC Bw. Muungano Kasibi Saguya alipowatembelea ili kujuwa changamoto zinazowakabili. Kikundi hicho kimeshapata kazi za watu binafsi na shule ili kuwajengea majengo mbalimbalia na hivyo kupata fedha za kujiendeleza. Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya Vijijini imekubali kuwapa vijana hao ardhi na maeneo ya kufanyia kazi.
New Picture (4)
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje Bw. James Milanzi akimsikilza Meneja wa Huduma kwa Jamii wa NHC Bw. Muungano Saguya alipofika Ofisini kwake kukumbusha wajibu wa Halmashauri za Wilaya wa kusaidia vijana ili waweze kutengeneza matofali ya kujengea nyumba za gharama nafuu na kujipatia ajira. Halmashauri hiyo imepiga marufuku ukataji miti kwa ajili ya kuchoma matofali na badala yake wananchi wametakiwa kutumia matofali rafiki wa mazingira yanayozalishwa kwa kutumia mashine zilizotolewa na NHC kama msaada kwa vijana katika Halmashauri zote nchini.

No comments:

Powered by Blogger.