Header Ads

ZIARA YA KATIBU MKUU NDANI YA JIMBO LA MAGU LEO,KESHO KURINDIMA JIMBO LA NYAMAGANA JIJINI MWANZA.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza Bw. Miraji Mtaturu kushoto wakionyesha magwanda yaliokabidhiwa kwao aiyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wilaya ya Magu,Bi. Juliana Kachilu ambaye amejiunga na Chama cha Mapinduzi kutoka CHADEMA.Zaidi ya wananchama 53 kutoka vyama vya upinzani walijiunga na CCM wakiwemo Chadema 28 na ACT 12 na wengine kutoka vyama vingine.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokea magwanda ya aliyekuwa  Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA (BAWACHA) Wilayani Magu  Bi. Juliana Kachilu ambaye amejiunga na Chama cha Mapinduzi, kushoto ni Katibu wa CCM mkoa wa Mwanza Bw. Miraji Mtaturu.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyesha kadi zilizokuwa  za wanachama wa chama cha Demokrasia na Maendeleo na vyama vingine mara baada ya wanachama hao kujiunga na CCM katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kituo cha mabasi cha Kisesa wilayani Magu mkoani Mwanza.

Katibu Mkuu huyo amempokea aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake la CHADEMA (BAWACHA) Wilayani Magu  Bi. Juliana Kachilu ambaye amejiunga na Chama cha Mapinduzi , Kinana yuko katika ziara ya kikazi  ya mkoa Mwanza akimalizia mkoa wa mwisho wa Tanzania baada ya kuzunguka mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani akipita katika majimbo yote, wilaya zote hapa nchini  na nusu ya Kata na vijiji kwa muda wa miaka miwili akikagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010-2015.

Kinana amesikiliza kero mbalimbali za wananchi na kuzipatia ufumbuzi huku akihimiza uhai wa CCM ambapo pia  katika ziara hiyo amekuwa akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Nape Nnauye . 
Baadhi ya Kadi za wafuasi wa vyama mbalimbali walizoamua kuachia ngazi na kuhamia chama CCM.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mkuu wa mkoa wa Mwanza Ndugu Magesa Mulongo wakifungua maji kama ishara ya uzinduzi wa utumiaji wa maji hayo katika mji wa Magu. 
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Magu. Katika Kikao hicho Katibu Mkuu wa CCM amewajia juu Viongozi wanaotumia vibaya nafasi zao kwa kujifanya maarufu zaidi ya Chama alisema "Hakuna mtu maarufu zaidi ya CCM huku akisema kuna watu wanaona kama wamekiteka hiki chama nyara na kukiweka kwenye kikapu na kuzunguka nacho, Hatutokubali hilo litokee" aliendelea kusema bora mtu aende upinzani kulikoni kuwa na sisi halafu anatuumiza. 

 Mkuu wa mkoa wa Mwanza Ndugu Magesa Mulongo akizungumza na wananchi kuhusu kuiagiza mamlaka ya Mapato TRA na kikosi cha Usalama Barabarani kuenda katika wilaya kwa ajili ya kutoa huduma za utoaji wa leseni za uendeshaji vyombo vya moto na kukusanya kodi mbalimbali za vyombo vya moto ili kupunguza urasimu wa huduma hiyo ambazo zimekuwa zikipatikana kwenye miji mikuu ya mikoa peke yake.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akimsikiliza mmoja wa wakazi wa Magu mjini,aliyekuwa akitoa kero yake kubwa ya upatikanaji wa maji katika eneo hilo,katika mkutanno wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa saba saba
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akijibu hoja mbalimbali zilizokuwa zimeulizwa na baadhi ya wakazi wa mji wa Magu mapema leo jioni katika mkutanno wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa saba saba
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akibeba tofari mara baada ya kushiriki kufyatua wakati alipokagua shughuli za kikundi hicho katika kijiji cha Irungu wilayani magu.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Kinana akzungumza jambo mara baada mara baada ya kukabidhi mashine kwa vijana wafyatua matofali katika kijiji cha Nyigoro-Ilungu wilayani Magu,ambapo vijana hao walipata tenda ya kujenga Nyumba ya Bibi Asteria Selemani inayojengwa na Mwanaye Zakaria Andrew katika kijiji cha Irungu wilayani Magu Anderw amekipatia tenda ya kufyatua matofali ya kujengea nyumba hicho kikundi cha vijana ambacho  kimefadhiliwa mashine ya kufyatua matofali na Shirika la Nyumba Tanzania NHC.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa Mhandisi wa maji wa Wilaya ,Injinia Rutta Merchades alipotembelea chanzo cha maji Nyanguge wilayani Magu.
 Wakazi wa Nyanguge wakisubiri maji kuzinduliwa na katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ambaye yupo kwenye ziara ya mkoa wa Mwanza ya kukagua ,kuhimiza na kusukuma utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka jiwe la msingi la uzinduzi wa mradi wa Maji Nyanguge.
  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimtwisha ndoo ya maji kama ishara ya kuzinduliwa kwa huduma za maji Bi.Yustina mkazi wa Nyanguge.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsalim fundi Raina Lucas anayeshiriki ujenzi wa jengo la x-ray katika kituo cha afya Kisesa.
 Pichani ni moja ya jengo la X-Ray linalojengwa  katika kituo Afya Kisesa wilayani Magu.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu  Kinana akiwahutubia wakazi wa mji wa Kisesa mapema jioni ya leo alipokuwa akimaliza ziara yake ndani ya jimbo la Magu.

No comments:

Powered by Blogger.