CHAMA CHA WAFANYAKAZI MADEREVA TANZANIA (TADWU), CHAMKABIDHI MLEZI WAO MKUU WA WILAYA YA KINONDONI PAUL MAKONDA RASIMU YA MKATABA WA MABORESHO YA MASLAHI YAO.
Mlezi
wa chama cha wafanyakazi madereva Tanzania (TADWU), Mkuu wa Wilaya ya
Kinondoni, Paul Makonda (katikati), akizungumza na madereva kabla ya
kukabidhiwa rasimu ya maboresho ya maslahi ya madereva hao na cheti cha
utambulisho wa chama hicho Dar es Salaam jana. Kulia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU), Abdallah Lubara na Mwenyekiti wa zamani wa Umoja wa Madereva Tanzania, Clement Masanja.
Katibu
Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU), Abdallah
Lubara (kulia), akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda,
rasimu ya mkataba wa maslahi ya madereva waliyokuwa wakiidai serikali
kwa muda mrefu Dar es Salaam jana.
Mwenyekiti
wa zamani wa Umoja wa Madereva Tanzania, Clement Masanja (kushoto),
akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda cheti cha
utambulisho wa chama chao kipya kitakachoitwa Chama cha Wafanyakazi
Madereva Tanzania (TADWU) baada kuundwa rasmi ambacho kitazindulia Julai
Mosi mwaka huu.
Naibu katibu mkuu wa chama hicho, Rashid Said (kulia) akizungumzia yaliyomo kwenye rasimu hiyo na maboresho ya maslahi yao.
DC Makonda akisalimiana na madereva baada ya kumaliza kwa mkutano huo.
No comments:
Post a Comment