Header Ads

CHAMA CHA WAFANYAKAZI MADEREVA TANZANIA (TADWU), CHAMKABIDHI MLEZI WAO MKUU WA WILAYA YA KINONDONI PAUL MAKONDA RASIMU YA MKATABA WA MABORESHO YA MASLAHI YAO.

 Mlezi wa chama cha wafanyakazi madereva Tanzania (TADWU), Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (katikati), akizungumza na madereva kabla ya kukabidhiwa rasimu ya maboresho ya maslahi ya madereva hao na cheti cha utambulisho wa chama hicho Dar es Salaam jana. Kulia ni  Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU), Abdallah Lubara na Mwenyekiti wa zamani wa Umoja wa Madereva Tanzania, Clement Masanja.
 Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU), Abdallah Lubara (kulia), akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda, rasimu ya mkataba wa maslahi ya madereva waliyokuwa wakiidai serikali kwa muda mrefu Dar es Salaam jana.

Mwenyekiti wa zamani wa Umoja wa Madereva Tanzania, Clement Masanja (kushoto), akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda cheti cha utambulisho wa chama chao kipya kitakachoitwa Chama cha Wafanyakazi Madereva Tanzania (TADWU) baada kuundwa rasmi ambacho kitazindulia Julai Mosi mwaka huu.
 Naibu katibu mkuu wa chama hicho, Rashid Said (kulia) akizungumzia yaliyomo kwenye rasimu hiyo na maboresho ya maslahi yao.
 DC Makonda akisalimiana na madereva baada ya kumaliza kwa mkutano huo.
 Madereva wakiwa wamesimama wakisubiri kusalimiana na mlezi wao DC Paul Makonda.

No comments:

Powered by Blogger.