Header Ads

MFUMUKO WA BEI WAONGEZEKA NCHINI

1
Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bw. Ephraimu Kwesigabo akitoa taarifa ya kuongezeka kidogo kwa mfumuko wa bei nchini kwa mwezi Mei 2015 leo jijini Dar es salaam.Mfumuko wa Bei  kwa mwezi Mei,2015 umefikia asilimia 5.3  kutoka asilimia 4.5 iliyokuwepo mwezi Aprili, 2015.
3
Waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo leo.
…………………………………………………………………..
Na. Aron Msigwa – MAELEZO.
 
Ofisi ya Taifa ya Takwimu imesema kuwa Mfumuko wa Bei wa Taifa kwa mwezi Mei 2015 umeongezeka hadi kufikia asilimia 5.3 kutoka asilimia 4.5 ya mwezi Aprili 2015 kutokana na kuongezeka kwa kasi ya upandaji wa bei ya  bidhaa na huduma katika maeneo mbalimbali nchini.

Mkurugenzi wa sensa ya Watu na Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Ephraim Kwesigabo akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam amesema kuwa kuongezeka kwa mfumuko wa Bei nchini kumesababishwa na kasi ya upandaji wa bei ya bidhaa za vyakula zinazotumiwa kwa wingi na kaya binafsi kwa mwezi Mei.

Amesema bidhaa za vyakula na zile zisizo za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko huo ni  Nyama,Choroko, Maharage,samaki, nyama,unga wa mihogo.

Kwa upande wa bidhaa zisizo za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfumuko wa bei ni bei za mavazi ya wananume kwa asilimia 5.6, mavazi ya wanawake kwa asilimia 3.5, vyakula kwenye migahawa kwa asilimia 4.1 na huduma za malazi kwa asilimia 4.2.

No comments:

Powered by Blogger.