Header Ads

HOTUBA YA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA (Mb) KWENYE MKUTANO WAKUTANGAZA NIA YA KUWANIA URAIS‏


Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa ahutubia wananchi kwenye Mkutano wa hadhara, wakati akitangaza nia yake ya kuwania Urais wa Awamu wa tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM.
--------
HOTUBA YA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA (Mb) KWENYE MKUTANO WA KUTANGAZA NIA YA KUGOMBEA URAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KUPITIA CCM
UTANGULIZI:
Ndugu viongozi, wana-CCM na Watanzania wenzangu; Kwanza nianze kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetufikisha hapa leo.  Lakini pia niwashukuru nyote mlioweza kufika hapa leo.  Kipekee niwashukuru CCM wenzangu na Watanzania kiujumla ambao wameendelea kuwa marafiki na kuniuunga mkono.…
Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mh. Edward Lowassa ahutubia wananchi kwenye Mkutano wa hadhara, wakati akitangaza nia yake ya kuwania Urais wa Awamu wa tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM.
--------
HOTUBA YA MHESHIMIWA EDWARD LOWASSA (Mb) KWENYE MKUTANO WA KUTANGAZA NIA YA KUGOMBEA URAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA KUPITIA CCM
UTANGULIZI:
Ndugu viongozi, wana-CCM na Watanzania wenzangu; Kwanza nianze kumshukuru Mwenyezi Mungu aliyetufikisha hapa leo.  Lakini pia niwashukuru nyote mlioweza kufika hapa leo.  Kipekee niwashukuru CCM wenzangu na Watanzania kiujumla ambao wameendelea kuwa marafiki na kuniuunga mkono. Hakika nimejawa na furaha.
Hii ni siku muhimu kwangu na kwa nchi yetu. Leo nimeamua kuwaita ili kuwatangazia rasmi azma yangu ya kuomba ridhaa ya chama chetu, Chama Cha Mapinduzi (CCM), ili niteuliwe kukiwakilisha cha chetu kuwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Naamini historia itaihifadhi kama ni siku ambayo kwa mara ya pili katika maisha yangu, nimejitokeza kuwania kuiongoza nchi yetu kupitia chama chetu. Mara ya kwanza ilikuwa ni mwaka 1995 wakati wa uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi hapa nchini nilipojitokeza nikiwa pamoja na Rais Jakaya Kikwete;
Wakati ule sote tulikuwa wanasiasa vijana. Pamoja tulikwenda kuchukua fomu na baadaye kwa pamoja tukazungumza na waandishi wa habari. Tulileta hamasa kubwa pale tulipofanya jambo ambalo halikuzoeleka kwa Watanzania kwa kutangaza kwamba yeyote atakayepita kati yetu, mwenzake ambaye hatafanikiwa angemuunga mkono.
Ningeweza kujitokeza tena mwaka 2005 lakini nikaamua kwa dhati kumuunga mkono Rais Jakaya Kikwete.
Nikiwa Mwenyekiti wa Kampeni niliwaongoza wenzangu kufanikisha ushindi mkubwa wa mgombea wetu, na baadaye ushindi mkubwa wa asilimia 80 kwa Chama Cha Mapinduzi kwenye uchaguzi mkuu wa 2005.
Nitaeleza kwa nini nimeamua kujitokeza tena, na kwa nini naamini mimi ndiye mtu sahihi wa kuiongoza nchi yetu wakati huu. Mpaka hapa itoshe tu kuwaeleza ni kwa nini naamini leo ni siku muhimu. Ni siku muhimu kwa sababu nina kiu ya kuona Watanzania wenzangu tunajiunga kuianza safari ya matumaini.
Ni siku muhimu kwa nchi yetu pia, kwa sababu naamini inajibu wito wa mahitaji ya sasa ya uongozi wa Taifa letu wa kumpata kiongozi imara atakayewaongoza Watanzania kujenga taifa imara. Na hili nitalieleza kwa kina. Hii ndiyo safari ya matumaini.
CLICK HAPA KU-DOWNLOAD HOTUBA KAMILI===>

No comments:

Powered by Blogger.