Header Ads

URITHI WA UTAMADUNI WAELEZWA KUWA KIVUTIO MUHIMU CHA UTALII NCHINI

  Mkurugenzi Uendeshaji na Utumishi wa Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo Joseph Kilangi akitoa hutuba yake ya ufunguzi katika Semina ya majadiliano ya “Rasimu ya Sera ya Urithi wa Utamaduni” iliyofanyika Forodhani Mjini Zanzibar,kulia kwake ni Mkurugenzi wa Uendeshaji na Utumishi, Sera na Utafiti wa Wizara hiyo na kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale Dkt. Amina Ameir Issa. 
 Proff Shariff Mtaalamu wa Historia akitoa mchango wake katika Semina ya majadiliano ya ‘Rasimu ya Sera ya Urithi wa Utamaduni’ iliyofanyika Forodhani Mjini Zanzibar. 
 Mwalimu wa Historia Chuo Kikuu cha Taifa Suza Bi Zainab Othman akitoa mawazo ya kuiboresha Rasimu hiyo katika Semina ya kuijadili ‘Rasimu ya Sera ya Urithi wa Utamaduni’ Semina hiyo iliyofanyika Forodhani Mjini Zanzibar.
 Mjumbe kutoka Jumuiya ya Uokozi Zanzibar Omar Kombo akiijadili ‘Rasimu ya Sera ya Urithi wa Utamaduni’ katika Semina iliyofanyika Forodhani Mjini Zanzibar. Semina hiyo ya Siku mbili imefanyika kwa lengo la kupata maoni tofauti kutoka kwa Wadau mbalimbali nchini. Picha na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar. 
 Mkurugenzi wa Sanaa Zanzibar Mdungi Ussi akichangia Rasimu ya Sera ya Urithi wa Utamaduni ambapo pamoja na mambo mengine ameshauri Sera hiyo isiingiliane na Sera zingine.Picha na Faki Mjaka
  Mkurugenzi wa Idara ya Makumbusho na mambo ya kale Dkt Amina Ameir Issa akiwashukuru Washiriki kwa michango yao katika Semina ya Majadiliano ya Rasimu ya Sera ya Urithi wa Utamaduni iliyofanyika Forodhani mjini Zanzibar,kulia kwake ni Mkurugenzi wa Uendeshaji, Sera na Utafiti wa Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar Mashaka Hassan Mwita na kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Magofu Zanzibar Abdallah Khamis Magofu-Picha na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar
 Mkurugenzi wa Uendeshaji, Sera na Utafiti wa Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar Mashaka Hassan Mwita katikati akifunga Semina ya Majadiliano ya Rasimu ya Sera ya Urithi wa Utamaduni iliyofanyika Forodhani mjini Zanzibar,kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Makumbusho na Mambo ya kale Dkt Amina Ameir Issa na kulia ni Makamu Mwenyekiti ZATO Hassan Ali Mzee.

No comments:

Powered by Blogger.