MSAMA AWATAKA WAIMBAJI WA MUZIKI WA INJILI KUFANYA KAZI YA MUNGU NA SI MAMBO YA SIASA.

MKURUGENZI
wa Kampuni ya Msama Promotions ambayo ndio inaandaa matamasha ya Pasaka
na Krismasi, Alex Msama amekemea waimbaji wa muziki wa Injili Tanzania
kufanya kazi ya Mungu na kuachana na siasa ambazo zinawaondoa kwenye
uinjilishaji.
Msama
ameyasema hayo wakati tukielekea kwenye uchaguzi Mkuu wa Madiwani,
Wabunge na urais unaotarajia kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Msama
anasema karipio hilo linawahusu pia viongozi wa dini wakiwamo
Wachungaji na Maaskofu ambao wanaonesha nia ya kutaka kuwania uongozi
wa kisiasa katika nafasi hizo tatu.Sababu
za Msama kukemea waimbaji wa Injili kujihusisha na Wanasiasa wakiwemo
wagombea urais, kuna baadhi ya waimbaji wametunga nyimbo za ‘kuwatukuza’
wagombea urais wakati wao wanatakiwa muda wote kumtukuza Mungu na si
binaadam wenzao.
“Waimbaji
tunatoka katika mstari, kwani Mungu anawategemea kufikisha ujembe wake
kwa lengo la kuachana na machukizo ambazo yanapoteza mwelekeo wa jamii
mbalimbali ambazo zinahitaji maono ya Wainjilisti,” alisema Msama na
kuongeza. “Waimbaji
ambao ninashirikiana nao katika kufikisha huduma ya neno la Mungu,
nashangaa wanatoka katika mstari nawaomba wamrudie Mungu kwani wanapotea
wakiwatumikia mabwana wengine.” Alisema.
Anasema
kitendo wanachokifanya waimbaji na wachungaji ni kinyume na huduma
ndani ya mioyo yao kwa sababu wanachokifanya si sahihi. Anafafanua
kwamba kazi ya muziki wa injili ni kuhubirisha, waimbaji ni Wainjlisti
wanawatoa waovu kwa shetani na kuwapeleka kwa Mungu ambaye ndiye
tegemezi kwa binadamu wote.
No comments:
Post a Comment