Header Ads

JAMBO LEO YAICHABANGA BODABODA FC TAMASHA LA BODABODA UKONGA

 Mlinda mlango Maganga Benjamin wa timu ya Bodaboda Wilaya ya Ilala, akiudaka mpira katikati ya wachezaji wa timu ya Jambo Leo 'Wagumu Stars' Zahoro Mlanzi (kushoto) na Ali Salum wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam. Mgeni rasmi katika tamasha hilo alikuwa Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa. Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.
 Mchezaji wa timu ya Jambo Leo,  Frank Balile (kushoto) akiwania mpira na mchezaji wa timu ya Bodaboda, Sharif Mohamed
 Moja ya kizazaa langoni mwa Bodaboda FC iliyosababishwa na washambuliaji wa Jambo Leo
 Mshambuliaji wa timu ya Gazeti la Jambo Leo, Ali Salum (katikati) akifunga bao la kwanza dhidi ya Bodaboda FC,wakati wa Tamasha la Bodaboda lililofanyika kwenye Uwanja wa Ukonga Gerezani, Dar es Salaam leo. Mgeni rasmi katika tamasha hilo alikuwa Meya wa Manispaa ya Ilala, Jerry Silaa.Jambo Leo ilishinda mabao 2-1.

No comments:

Powered by Blogger.