Header Ads

ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM NDUGU KINANA NA UJUMBE WAKE NDANI YA JIMBO LA LONGIDO MKOANI ARUSHA.


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokea kadi na bendera za aliyekuwa Katibu Mwenezi wa Chadema Wilaya ya Longido ambaye amejiunga na CCM kwenye mkutano uliofanyika Eworendeke.Ndugu Kinana akiwa ameongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wako kwenye ziara ya siku tisa mkoani Arusha ya Kuhimiza,kuimarisha na kutekeleza Ilani ya uchaguzi ya ccm ya mwaka 2010 ikiwemo pia na kusikiliza matatizo ya Wananchi na kuyapatia ufumbuzi.
Wananchi wa kijiji cha Eworendeke wakiwa wamekusanyika wakimsikiliza
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana alipokuwa akiwahutubia wilayani humo.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Eworendeke ambapo alitoa salaam za shukrani kwa CCM wilaya ya Longido kwa kuipa ushindi mzuri wakati wa uchaguzi.
Wananchi wakisikiliza hotuba kwa makini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa ujenzi

  wa nyumba ya watumishi wa Afya katika kijiji cha  Lesingeita,wilayani Longido.Pichani shoto ni Mbunge wa jimbo la Longido Mh.Lekule Laizer.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Eworendeke ambapo alimpongeza mbunge wa jimbo la Longido kwa uamuzi wake wa kutogombea uchaguzi ujao na kusema wanasiasa wengi wanajua kuingia kwenye siasa lakini wakisahingia hawajui wakati gani wa kutoka.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi
wa Kijiji cha Engikareti wilaya Longido.
Mzee Kitasho Simel Nakutamba akimpa mkono Katibu Mkuu wa CCM ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika hoteli yake ya Longido kama ionekanavyo pichani.
Pichani ni jengo la kituo cha mafunzo cha Learning In Longido (LIL),ambapo  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana aliweka jiwe la msingi na kushiriki kupaka rangi kwenye majengo hayo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupaka rangi kwenye majengo ya kituo cha mafunzo cha Learning In Longido (LIL).



Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiandaa sindano ya
chanjo tayari kwa kumchoma ng'ombe.,Pichani shoto ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha,Ndugu Onesmo Ole Nangolo akishuhudia tukio hilo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kumchoma ng'ombe chanjo kwenye mradi wa ufugaji wa madume bora katika kijiji cha Ketumbeine.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kama ishara ya ufunguzi wa jengo la hoteli katika kijiji cha Kitumbeine,kushoto ni mmiliki wa hoteli hiyo Ndugu Halifa Juma.
Mbunge wa Viti Maalumu Vijana,Catherine Magige akiwahutubia wakazi wa Eworendeke,Wilayani Longido.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na vijana wa kimasai alipowasili  kwenye kituo cha mafunzo Learning In Longido

No comments:

Powered by Blogger.