TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO WA WAWEKEZAJI NA MARAIS WA NCHI 5 ZA AFRIKA MASHARIKI.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam akitoa taarifa ya mkutano
wa wawekezaji (Round Table Investment Forum) na wakuu wa nchi 5 za
ukanda wa Afrika Mashariki utakaofanyika jijini Dar es salaam
kuanzia Machi 25 hadi 26 mwaka huu.
![]() |
Kamishina wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova akitoa taarifa ya hali ya ulinzi na usalama katika jiji la Dar es salaam na vifo vya watu 7 waliopoteza maisha kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika jiji la Dar es salaam. |
Na Aron Msigwa –MAELEZO.
Tanzania
inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mkutano wa wawekezaji (Round Table
Investment Forum) na Marais wa nchi 5 za ukanda wa Afrika Mashariki
utakaofanyika jijini Dar es salaam kuanzia Machi 25 hadi 26 mwaka huu.
Akitoa
taarifa ya mkutano huo Mkuu wa wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Saidi Meck
Sadiki amesema kuwa Marais hao Paul Kagame wa Rwanda, Pierre
Nkurunzinza wa Burundi, Yoweri Museveni wa Uganda, Uhuru Kenyatta wa
Kenya na Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo watahudhuria
mkutano huo wakiwa wameambatana na jumla ya wawekezaji 350.
Amesema
Tanzania kwa mara nyingine imepata heshima ya kuandaa mkutano huo na
kufafanua kuwa wawekezaji hao wamekwisha anza kuwasili jijini Dar es
salaam kuanzia Machi 22 , Machi huku marais nchi hizo wakitarajiwa
kuwasili jijini humo kuanzia Machi 24,2015.
No comments:
Post a Comment