SIMBACHAWENE AIOMBA BENKI YA DUNIA KUISAIDIA TANESCO

……………………………………………………………………………….
Na Greyson Mwase, Dar es Salaam
Waziri
wa Nishati na Madini, George Simbachawene ameliomba Shirika la Fedha
Duniani (WB) kulisaidia Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) ili liweze
kuimarisha miradi ya usambazaji wa umeme nchini hususan vijijini.
Simbachawene aliyasema hayo wakati alipokutana na ujumbe kutoka Benki ya Dunia na watalaam wa Wizara ya Nishati na Madini ili kujadili maendeleo ya miradi ya nishati nchini inayofadhiliwa na Benki hiyo, changamoto zake na kupata mapendekezo ya kuboresha miradi hiyo.
Simbachawene aliyasema hayo wakati alipokutana na ujumbe kutoka Benki ya Dunia na watalaam wa Wizara ya Nishati na Madini ili kujadili maendeleo ya miradi ya nishati nchini inayofadhiliwa na Benki hiyo, changamoto zake na kupata mapendekezo ya kuboresha miradi hiyo.
Alisema
kuwa Tanesco inakabiliwa na changamoto ya fedha katika utekelezaji wa
miradi ya umeme hususan usambazaji wa umeme vijijini na kupelekea miradi
mingi kutokamilika kwa wakati.
Akielezea
maendeleo ya shirika hilo la umeme, Simbachawene alisema kuwa shirika
hilo limeongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato kwa kubuni mikakati
mbalimbali ya ukusanyaji wa mapato hayo na kupunguza hasara zilizokuwa
zikijitokeza mara kwa mara.
Akielezea
kuhusu upunguzaji wa bei ya umeme nchini, Simbachawene alisema kuwa
Serikali imejenga bomba kubwa la gesi kutoka Mtwara hadi jijini Dar es
Salaam jambo litakalochangia upatikanaji wa nishati ya umeme ya uhakika
na kwa gharama nafuu ambalo ni moja ya utekelezaji wa Mpango wa Matokeo
Makubwa Sasa.
“
Ili kuhakikisha wananchi wananufaika na sekta mpya ya gesi, serikali
ilibuni utaratibu wa kusomesha wataalam pamoja na wanafunzi waliofanya
vizuri katika masomo ya sayansi katika vyuo vikuu vinavyotoa fani za
mafuta na gesi ili kuwa na wataalamu watakaosimamia kwa ufanisi sekta ya
gesi na mafuta.,” alisema Simbachawene .
Aliongeza
kuwa mara baada ya kuwa na wataalam waliobobea katika masuala ya gesi
na mafuta, serikali itaunda taasisi itakayokuwa na kazi ya kutoa ushauri
katika masuala ya gesi na mafuta hususan wakati wa uingiaji wa
mikataba.
No comments:
Post a Comment