Header Ads

RAIS KIKWETE AMPONGEZA RAIS MPYA WA NAMIBIA DKT.HAGUE GEINGOB

qqq
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Rais Mpya wa Namibia Dkt.Hage Geingob wakati wa sherehe za kuapishwa kwake zilizofanyika katika Uwanja wa michezo wa Uhuru wa Namibia jijini Windhoek leo.Sherehe za kumuapisha Rais huyo wa tatu wa Namibia ziligongana na maadhimisho ya miaka 25 ya uhuru wan chi hiyo.
(picha na Freddy Maro)
………………………………………………………………………………….
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumamosi, Machi 21, 2015, ameungana na viongozi mbalimbali wa Afrika na wananchi wa Namibia katika kusherehekea miaka 25 ya uhuru wa nchi hiyo na kuapishwa kwa Rais wa Tatu wa Namibia, Mheshimiwa Dkt. Hage Gotfried Geingob.
Mheshimiwa Geingob alikuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo kabla ya uchaguzi mkuu wa Novemba 28, mwaka jana, uliokipa ushindi mkubwa chama tawala cha SWAPO.
Katika sherehe kubwa na ya kufana iliyofanyika kwenye Uwanja wa Michezo wa Independence mjini Windhoek, Rais Kikwete ameshuhudia Namibia ikiadhimisha miaka 25 ya Uhuru wake na makabidhiano ya uongozi wa juu wa nchi hiyo kwa amani kwa mara ya pili katika historia yake.
Mheshimiwa Dkt. Geingob ameapishwa rasmi na Jaji Mkuu wa nchi hiyo, Mheshimiwa Peter Shivute saa sita na dakika 25 kwa saa za Afrika Mashariki, kiapo ambacho kilifuatiwa na kiapo cha Makamu wa Rais, Waziri Mkuu na Naibu Waziri Mkuu.
Ujumbe wa Tanzania katika sherehe hizo uliwashirikisha pia marais wa zamani, Mzee Ali Hassan Mwinyi na Rais Ben Mkapa, ambao wote waliwasili mjini Windhoek usiku wa jana kwa ndege maalum ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

No comments:

Powered by Blogger.