Header Ads

Muswada wa Sheria ya Udhibiti wa Umiliki Silaha wasomwa kwa mara ya Pili Bungeni

bu Waziri  wa Mambo ya Ndani Mhe.Pereira Silima amesoma Muswada wa Sheria ya Kupendekeza kutungwa kwa  Sheria ya Usimamizi na Udhibiti wa Silaha ya mwaka 2014 Bungeni Dodoma kwa mara ya pili tarehe 19 Machi 2015.
Mhe.Silima alisema Serikali imeona umuhimu wa kutunga Sheria hii ya Udhibiti wa  Umiliki wa silaha kutokana na kukabiliana na tatizo la kuwepo na watu wengi wanao kumiliki silaha kinyume na sheria pamoja na kufanya matumizi mabaya ya silaha.
“Serikali imekubaliana na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa na mfumo wa kisheria baada ya kusaini na kuridhia maazimio ya kudhibiti uzagaaji wa  silaha haramu na sheria hii inaelekeza wazi kuwa mtu anaweza kumiliki silaha akiwa na umri wa kuanzia miaka 25,”alisema Mhe.Silima.
 Mhe.Silima aliendelea kusema kuanzia mwaka 2000 mpaka 2013 serikali ilikamata zaidi ya silaha 34,156 zilizokamatwa katika operesheni mbalimbali na silaha hizo ziliteketezwa.
Kwa upande wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ulinzi na Usalama inayoongozwa na Mhe.John Chiligati aliipongeza serikali kupitia kifungu chake cha 19 kinachoeleza kuwa sihala zote zitawekwa alama ya utambuzi wa kitaifa,Pia baada ya sheria hii kupitishwa suala hilo lizingatiwe.  
“Kamati inapenda kuishauri Serikali katika kifungu cha 20(2) kuondoa adhabu ya kulipa faini kwa mtu anayemiliki silaha kinyume na sheria na badala yake ni kutumikia kifungu kisichozidi miaka mitano”,alisema Mhe.Chiligati.
Mhe.Chiligati aliendelea kusema kamati imeridhia marekebisho ya Serikali ya kuongeza idadi ya wajumbe wa kamati ili iwe na uwakilishi mpana  kutoka sekta binafsi,Pia Kamati imeshauri kifungu cha 5(3) kisomeke  kuwa mtu yeyote atakuwa na sifa za kuteuliwa kuwa mjumbe wa kamati endapo ni raia wa Jamhuri ya Muungano.
Naye Mbunge wa Nkasi Kusini Mhe.Desderius Mipata ameipongeza Serikali kwa kuunda Sheria itakayo dhibiti umiliki wa silaha  nchini, pia ameishauri serikali kuangalia ni namna gani itadhibiti maduka yanayouza silaha nchini.

No comments:

Powered by Blogger.