WAKANDARASI UMEME WASIOWAJIBIKA KUNYANG’ANYWA TENDA
Waziri
wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Meza Kuu-Katikati), akizungumza
na wawakilishi wa Kampuni mbalimbali zinazohusika kusambaza umeme vijijini
kutoka India, China na Sri Lanka zinazofanya kazi katika Mikoa ya Nyanda za Juu
Kusini kuhusu utekelezaji wa miradi husika. 
Wawakilishi
wa Kampuni mbalimbali zinazohusika kusambaza umeme vijijini kutoka India, China
na Sri Lanka zinazofanya kazi katika Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini Magharibi
pamoja na baadhi ya Mameneja wa Tanesco wa Mikoa husika, wakitoa mrejesho kwa
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Meza Kuu – Katikati),
kuhusu hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Miradi husika. Kulia kwa Waziri
Muhongo ni Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Charles
Kitwanga na kushoto kwa Waziri ni Kamishna Msaidizi wa Nishati sehemu ya Umeme,
Mhandisi Innocent Luoga.
Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Umeme Vijijini
(REA), Dk. Lutengano Mwakahesya akizungumza katika mkutano baina ya Waziri wa
Nishati na Madini na kampuni zinazosambaza umeme vijijini kwa Mikoa ya Nyanda
za Juu Kusini. Mwakahesya aliahidi kushirikiana na wadau mbalimbali ili
kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa kiwango kinachotakiwa.
No comments:
Post a Comment