Header Ads

WAKANDARASI UMEME WASIOWAJIBIKA KUNYANG’ANYWA TENDA

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Meza Kuu-Katikati), akizungumza na wawakilishi wa Kampuni mbalimbali zinazohusika kusambaza umeme vijijini kutoka India, China na Sri Lanka zinazofanya kazi katika Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kuhusu utekelezaji wa miradi husika.
Wawakilishi wa Kampuni mbalimbali zinazohusika kusambaza umeme vijijini kutoka India, China na Sri Lanka zinazofanya kazi katika Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini Magharibi pamoja na baadhi ya Mameneja wa Tanesco wa Mikoa husika, wakitoa mrejesho kwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (Meza Kuu – Katikati), kuhusu hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Miradi husika. Kulia kwa Waziri Muhongo ni Naibu Waziri wa Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Charles Kitwanga na kushoto kwa Waziri ni Kamishna Msaidizi wa Nishati sehemu ya Umeme, Mhandisi Innocent Luoga.
 Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA), Dk. Lutengano Mwakahesya akizungumza katika mkutano baina ya Waziri wa Nishati na Madini na kampuni zinazosambaza umeme vijijini kwa Mikoa ya Nyanda za Juu Kusini. Mwakahesya aliahidi kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kwa kiwango kinachotakiwa.

No comments:

Powered by Blogger.