Umoja wa Machifu Tanzania (UMT) wawasilisha mapendekezo yao kuhusiana na Rasimu ya Katiba Mpya.
Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la
Katiba, Mhe. Samia Suluhu akiwaeleza jambo Wawakilishi wa Umoja wa Machifu
Tanzania (UMT) kuhusu mapendekezo yao waliyoyawasilisha kwake kwaajili ya
Katiba Mpya.
Chifu John Nyanza (aliyekaa katikati)
wa kutoka Magu akimueleza jambo Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba,
Mhe. Samia Suluhu (kulia) juu ya uwasilishaji wa mapendekezo yao kwa ajili ya
Katiba Mpya alipokutana naye leo kwenye Ofisi ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge
Maalum.
Chifu Agnes Ndaturu (kushoto) wa
kutoka Ntuzu, Bariadi akimueleza jambo Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la
Katiba, Mhe. Samia Suluhu (kulia) juu ya uwasilishaji wa mapendekezo yao kwa
ajili ya Katiba Mpya alipokutana naye leo kwenye Ofisi ya Makamu Mwenyekiti wa
Bunge Maalum.
Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la
Katiba, Mhe. Samia Suluhu (kulia) akipokea mapendekezo ya maoni toka kwa Chifu
John Nyanza alieuwakilisha Umoja wa Machifu wa Tanzania (UMT) leo kwenye Ofisi
ya Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum.
Baadhi
ya Waandishi wa Habari walikifuatilia uwasilishwaji wa mapendekezo toka kwa
Machifu waliouwakilisha Umoja wa Machifu wa Tanzania (UMT) leo kwenye Ofisi ya
Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum.
No comments:
Post a Comment