SERIKALI YAKUSANYA TAKRIBANI SHILINGI BILIONI 3 KUTOKANA NA KUONGEZEKA KWA MAKUSANYO YA MRAHABA WA MADINI
Mkurugenzi
wa Fedha na Utawala kutoka Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA)
Bruno Mteta akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam
kuhusu mafanikio yaliyopatikana baada ya ongezeko la makusanyo ya
mrabaha kwenye madini ya ujenzi kwa mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Udhibiti na Ukaguzi kutoka wakala huo Mhandisi
Liberatus Chizuzu.
……………………………………………………………
Frank Mvungi-Maelezo
SERIKALI imekusanya takribani shilingi bilioni 3 kutokana na kuongezeka
kwa makusanyo ya mrabaha uliotozwa katika madini ya Ujenzi katika mikoa
ya Dar es salaam na Pwani katika kipindi cha Juni mwaka 2011 hadi
Novemba mwaka 2013.
Hayo
yamesemwa na Mkurugenzi wa Utawala na Fedha wa wakala wa Ukaguzi wa
Madini Tanzania (TMAA) Bruno Mteta wakati wa mkutano na waandishi wa
habari leo jijini Dar es salaam.
Mteta
alisema awali kabla wakala huo haujaanza ukaguzi wa madini ya ujenzi
kiasi kilichokuwa kikikusanywa ni shilingi milioni tatu tu kwa mwaka
hivyo kwa sasa kiwango hicho kimefikia wastani wa Bilioni moja kwa
mwaka.
Alisema
ukaguzi umeimarishwa katika vituo vyote ambavyo wafanyabiashara
wanaojihusisha na biashara hiyo wanalazimika kupita na kuonyesha vibali
vya kusafirisha madini hayo ambavyo ni vocha maalum zinazotolewa na
wakala huo ili kudhibiti wale wanaokwepa kulipa mrabaha.
“Tumejipanga
vizuri kuhakikisha kuwa kila anayetakiwa kulipa mrabaha katika biashara
ya madini ya ujenzi anafanya hivyo kwa kuimarisha ukaguzi kupitia vituo
vyetu vya Afrikana,Pugu,Chalinze na katika maeneo yote yaliyobainishwa
kutumika katika uchimbaji wa madini ya Ujenzi” alisema Mteta.
Katika
hatua nyingine Mteta alisema kuwa ni wajibu wa kila mchimbaji na
mfanyabiashara wa madini kulipa mrabaha unaostahiki ambapo kifungu cha
87 (6) cha sheria ya Madini ya mwaka 2010 kinachotaka mrabaha ulipwe kwa
kuzingatia thamani halisi ya madini (gross value)yanapofikishwa sokoni
au kwa mtumiaji.
Naye Mkurugenzi wa udhibiti na Ukaguzi wa Uzalishaji na Biashara ya Madini Mhandisi Liberatus Chizuzu
alitoa wito kwa wananchi hasa wafanyabiashara wa madini ya ujenzi
kuzingatia sheria na kanuni za Madini ili kulisaidia Taifa kujenga
uchumi imara.
Wakala
wa Ukaguzi wa Madini Tanzania TMAA kwa kushirikiana na Ofisi ya
Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Mashariki ulianzisha matumizi ya
hati za mauzo ya Madini ya Ujenzi katika ukaguzi wa uzalishaji na mauzo
ya madini ya ujenzi Kanda ya Mashariki (Mikoa ya Dar es salaam na Pwani)
ambapo matumizi ya stakabadhi hizo yameongeza pato la Serikali kwa
kiasi kikubwa kutokana na makusanyo ya mrabaha kwa kiasi kikubwa.
No comments:
Post a Comment