Header Ads

KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA AKAGUA MIRADI MBALIMBALI YA MAENDELEO NA KUFANYA MKUTANO MKUBWA WA HADHARA WILAYANI NZEGA LEO


Katibu mkuu wa ccm,Ndugu Abdulrahman Kinana akipita kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo la mapokezi la wagonjwa wa nje (OPD),hospitali ya wilaya ya Nzega,mapema leo mchana,katika ziara yake anayoendelea nayo yenye lengo la kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na serikali sambamba na wananchi,ikiwemo pia kusikiliza kero za wananchi zinazowakabili na kuzitafutia majibu.
Katibu mkuu wa ccm,Ndugu Abdulrahman Kinana kulia na Mbunge wa jimbo la Nzega,Mh.Hamisi Kingwangalla wakishiriki katika ujenzi wa jengo la mapokezi la wagonjwa wa nje (OPD),hospitali ya wilaya ya Nzega,wakati Ndugu Kinana alipokagua ujenzi wa jengo hilo katika ziara yake anayoendelea nayo yenye lengo la kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na serikali sambamba na wananchi,ikiwemo pia kusikiliza kero za wananchi zinazowakabili na kuzitafutia majibu.
Katibu mkuu wa ccm,Ndugu Abdulrahman Kinana akioneshwa jambo kwenye simu na mfuasi wa chama cha CCM,mapema leo,wakati Ndugu kinana alipokwenda kushiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM kata katika kijiji cha Nkiniziwa,Wilayanni Nzenga mkoani Tabora. 
Katibu mkuu wa ccm,Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa Ofisi ya CCM kata katika kijiji cha Nkiniziwa,Wilayani Nzenga mkoani Tabora. 
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana pichani shoto na Katibu wa NEC Siasa,Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakimsikiliza mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari ya Kampala,Amos Kashindye namna ya kutumia moja ya kifaa cha maabara,mara baada ya kuitembelea shule hiyo ya kata na kukagua maabara ya sayansi na fizikia katika shule hiyo.
Katibu wa NEC Siasa,Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwahutubia wakazi wa kijiji cha Ndala katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Taifa,wilayani Nzega mkoani Tabora.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akikagua moja ya barabara zinazojengwa mjni Nzega kwa kiwango cha lami,kushoto kwake ni Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Nape Nnauye na pichani kati ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora,Mh,Fatma Mwasa.
Katibu wa NEC Itikadi,Siasa na Uenezi,Nape Nnauye akiyapokea baadhi ya mabango yaliyokuwa yamebebwa na baadhi ya vijana wanaojishughulisha na uchimbaji wa madini wilayani Nzega,wakiomba Serikali na chama cha CCM,kuwasaidia vijana hao wachimbaji wadogo wadogo kupewa maeneo yao ya kuchimba madini bila kubugudhiwa na mengineyo
Sehemu ya Wananchama na wafuasi wa chama cha CCM,wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika Nzega mjini mapema leo.
Nape Nnauye akiwahubia Sehemu ya Wananchana na wafuasi wa chama cha CCM,katika mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika Nzega mjini mapema leo.
Baadhi ya Baiskeli zilizotolewa na Mjumbe wa Mkutano Halmashauri kuu CCM Taifa,Ndugu Hussein Bashe kwa ajili ya kuwakabidhi viongozi wa mbalimbali wa chama hicho katika suala zima la kurahisha utendaji wao wa kazi. 
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiwahubia baadhi ya Wananchana na wafuasi wa chama cha CCM,katika mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika Nzega mjini mapema leo.
Sehemu ya Wananchama na wafuasi wa chama cha CCM,wakimsikiliza Katibu MKuu wa CCM,Ndugu Kinana (hayupo pichani) akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho uliofanyika Nzega mjini mapema leo.
Mkuu wa mkoa wa Tabora,Mh.Fatma Mwasa akizungumza jambo kwenye mkutano wa hadhara wa CCM,uliofanyika jioni ya leo Nzega Mjini.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akimpongeza Mjumbe wa Mkutano mkuu wa CCM,Taifa,Ndugu Hussein Bashe mara baada ya kukabidhi piki piki tatu kwa jumuiya za Chama,na Baiskeli 163 kwa ajili ya matawi yote ya CCM ya Wilaya ya Nzega kupitia mradi wao wa kuimarisha chama,pia alitoa baiskeli 37 kwa Jumuiya ya UVCCM wilayani humo,Pia alikabidhi kiasi cha shilingi Milioni mbili kwa kikundi cha Boda boda na milioni mbili kwa kikundi cha Mamalishe.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akimpongeza Mbunge wa Nzega,Mh.Hamisi Kingwangalla mara baada ya kukabidhi mashine ya kutotolea vifaranga kwa kikundi cha vijana.

No comments:

Powered by Blogger.