Header Ads

DAR YAZIZIMA KUFUATIA KIFO CHA BALOZI FLOSSIE GOMILE CHIDYAONGA

DSC_0051
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Zanzibar (Muungano na Utawala Bora), Mh. Mwinyi Haji Makame, akisaini kitabu cha maombolezo mara baada ya kuwasili kuhudhuria misa maalum ya kumwombea aliyekuwa Balozi wa Malawi nchini, Mh Flossie Gomile Chidyaonga kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es salaam.(Picha zote na Zainul Mzige wa MOblog).
DSC_0063
Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Zanzibar (Muungano na Utawala Bora), Mh. Mwinyi Haji Makame akibadilishana mawazo na Balozi wa Nigeria nchini Tanzania Dk Ishaya Samaila Majanbu (kushoto).
DSC_0099
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb), akiwasili kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es salaam akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. John Haule na kulakiwa na Makamu Balozi wa Malawi nchini Tanzania, Mh. Chisiza.
DSC_0106
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb), akisubiri kwenda kutia saini kitabu cha maombolezo kabla ya kuanza kwa ibada maalum ukumbini hapo. Kushoto ni Makamu Balozi wa Malawi nchini Tanzania, Mh. Chisiza.
DSC_0110
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb), akisaini kwa huzuni Kitabu cha Maombolezo kufuatia kifo cha aliyekuwa Balozi wa Malawi hapa nchini, Hayati Flossie Gomile-Chidyaonga kilichotokea Hospitali ya Aga Khan Jijini Dar es Salaam tarehe 09 mei 2014. Kulia ni Makamu Balozi wa Malawi nchini Tanzania, Mh. Chisiza.
DSC_0116 DSC_0123
Balozi wa Finland Tanzania, Sikka Antila wakilia kwa uchugu pamoja na Kaimu Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini, Bi .Joyce Mends-Cole wakati wa misa maalum ya kumwombea aliyekuwa balozi wa Malawi nchini Tanzania Mh. Flossie Gomile Chidyaonga kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere (JNICC) jijini Dar es salaam.

No comments:

Powered by Blogger.