Header Ads

SERIKALI KUONDOA TATIZO LA MAJI MKOA WA IRINGA

IMG_9499Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Uwezeshaji Dk. Mary Nagu akiwasili katika viwanja vya bunge mjini Dodoma mapema hii leo tayari kwa kuhudhuria mkutano wa kumi na tatu kikao cha nne.
IMG_9509Mbunge wa Kilolo Mh. Peter Msolla (kulia)akiingia katika ukumbi wa Bunge  hii leo tayari  kuhudhuria mkutano wa kumi na tatu kikao cha nne, katikati ni Mbunge wa Sikonge Mh. Said Nkumba na kushoto ni Mbunge wa Kigamboni Mh. Dk. Faustine Ndugulile.
Picha zote na Eliphace Marwa, MAELEZO Dodoma
Frank Mvungi-Maelezo Dodoma 
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imedhamiria kutatua tatizo la maji katika mji wa mafinga Mkoani Iringa ili kuwapa fursa wananchi kujiletea maendeleo kwa haraka.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri  Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mh. Kasim Majaliwa wakati akijibu swali la mbunge wa Mufindi Kaskazini mh.Mahmoud Hassan Mgimwa aliyetaka kujua hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuondoa tatizo la maji katika jimbo la Mufindi.
Alieleza kuwa mradi wa upanuzi wa mradi wa maji katika mji wa Mafinga unakadiriwa kugharimu zaidi ya shilingi bilioni 60 ambapo mradi huo utasaidia kuondoa tatizo hilo katika mji wa Mafinga.
Katika mradi huo Mh. Majaliwa alibainisha kuwa Serikali kupitia Wizara ya Maji imefanya usanifu wa mradi mkubwa ambao utahusisha ujenzi wa bwawa lenye ukubwa wa ujazo wa lita zipatazo milioni 2,800,000 ili kukidhi mahitaji yaliyopo.
Aidha Mh. Majaliwa aliongeza kuwa mradi huo utahusisha  ujenzi wa tanki 1 la mita za ujazo 1000 eneo la changarawe,Luganga tanki 1 la mita za ujazo 225 na mtula ujenzi wa tanki 1 la mita za ujazo 1000.
Pia Mamlaka ya Maji Mafinga kwa kushirikiana na Wizara ya Maji pamoja na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) ipo katika mpango wa kukopa kiasi cha zaidi ya milioni 300,000 kutoka katika taasisi za fedha kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji katika mji wa mafinga kwa kufanya upanuzi na uboreshaji wa miundombinu ya maji iliyopo.
Mji wa Mafinga una jumla ya wakazi 51,902 ambapo kabla ya kutekelezwa kwa mradi huu wananchi wanapoata huduma ya maji na salama ni asilimia 63

No comments:

Powered by Blogger.