ZANU-PF: WAAFRIKA VIPUUZENI VYAMA VYA UPINZANI
ZANU-PF: WAAFRIKA VIPUUZENI VYAMA VYA UPINZANI
*Chadai ni mawakala wa Nchi za Magharibi *Chahoji, kama Mugabe ni Mzee sana, mbona Malikia Elizabeth ni mzee zaidi ya Zimbabwe?
![]() |
| Katibu Mkuu, ZANU-PF,Mutasa, akizungumza leo |
BASHIR NKOROMO, DSM
Wametakiwa kuendelea kukiamini na kukiunga mkono Chama Cha Mapinduzi
(CCM), ili kiendelee kuongoza Tanzania kwa kuwa ndicho chama chenye sera
na mtazamo wa uhakika wa maendeleo.
WATANZANIA na Waafrika kwa jumla wametakiwa kutovitilia maanani vyama
vya upinzani kwa madai kuwa ni vya kibinafsi na havina mwelekeo wa
kuwasaidia wananchi.
Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu wa Chama tawala cha Zambia,
ZANU-PF, Didymus Mutasa, katika mkutano wa sita wa Makatibu Wakuu wa
Vyama vilivyokuwa vya ukjombozi kusini mwa Afrika, uliofanyika leo,
katika hoteli ya Kunduchi Beach, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Mutasa alisema vyama vya upinzani havina hadhi ya kuaminika sana kwa
wananchi kwa sababu si vyama makinikutokana na uanzishwaji wake kuwa ni
wa ubabaishaji jambo ambalo linavikosesha misingi ya kuweza kuleta
maendeleo.
“Afrika hakuna vyama vya upinzani, Watanzania wasikubali kabisa, kwa
kuwa vyama hivyo havina mwelekeo hasa kutokana na kutokuwa na mizizi
katika uanzishwaji wake tofauti na vyama utawala ambavyo pamoja na
kuanzishwa kwa lengo la kuzikomboa nchi zao lakini pia viliweka misingi
ya kuinua uchumi,’’alisema.
Alizilaum nchi za Magharibi, akisema ndizo zimeleta utitiri wa vyama
vya upinzani kwa lengo la kutafuta mianya ya kuja kunyonya na kupora
rasilimali zilizo ndani ya Afrika, na kusisitiza kuwa waafrika
wasikubali kuvipa nafasi.
Kuhusu chama chake cha ZANU-PF kuendelea kutwaa madaraka ya uongozi
nchini Zimbabwe kupitia chaguzi mbalimbali, ukiwemo ulimalizika hivi
karibuni na Rais Robert Mugabe kushinda Katibu Mkuu huyo alisema,
umetokana na Wazimbabwe kutokubali kuwapa wapinzani nchi na pia ZANU-PF
kusimamia vizuri sera ya uwekezaji.
“Tuna hakika tunapendwa na wazanzibabwe, hasa kutokana na serikali
kuwa wa wazi na kuhakikisha inasimamia rasilimali za nchi na hata
kusikiliza vilio vyao. Hivyo, ushindi wetu ni sauti ya Wazimbabwe,’’
alisema.
"Hata kelele zao hasa za kuhoji kuwa Rais Mugabe ni mzee mwenye umri
mkubwa, mbona wao wanasahau kuwa Malkia Elizabeth ni mzee kuliko hata
nchi yenyewe ya Zimbabwe achilia mbali Rais Mugabe?, alisema na
kuongeza;
“Malkia ni Mzee kuliko Zimbabwe yenyewe na bado ni malkia wa
Uingereza. Hivyo Mugabe ni Rais wetu na bado wazimbabwe wanampenda".
Akifungua mkutano huo, Mwenyekiti na mwenyekiti wa Mkutano huo,
Katibu Mkuu wa CCM, Abdurahman Kinana alisema miongoni mwa mambo ambayo
Makatibu wakuu watajadili kwa kina ni namna ya kuwatafutia fursa vijana,
ili waweze kushiriki katika masuala mbalimbali ya nchi zao ikiwemo
kushika nafasi za uongozi.
Vyama vilivyoshiriki Mkutano huo, ni CCM (Tanzania), SWAPO cha
Namibia, ZANU-PF cha Zimbabwe, MPLA cha Angola, FRELIMO cha Msumbiji na
ANC cha Afrika Kusini.

No comments:
Post a Comment