RAIS KIKWETE AZINDUA MIRADI kIBAHA,AHUTUBIA WANANCHI MLANDIZI
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa katika jiwe la msingi
wakati wa uzinduzi wa ujenzi wa jingo la Halmashauri ya mji wa Kibaha
leo.Kushoto ni Mbunge wa Kibaha mjini Mhe.Sylvestry Koka.
Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na mbunge wa Kibaha mjini Mhe.Sylvestry Koka
wakikagua jingo la Halmashauri ya mji wa Kibaha muda mfupi baada ya Rais
Kikwete kuweka jiwe la msingi huko mjini Kibaha leo.Rais Kikwete yupo
katika ziara ya kikazi mkoani Pwani.
Rais Kikwete akiwahutubia mamia ya wananchi katika Viwanja vya CCM,huko Mlandizi, Kibaha
Mwakilishi
wa Serikali ya Cuba ambaye pia ni Mkuu wa shirika la utafiti la
LABIOFAM Dr.Jose Antonio Fraga Castro(kushoto) pamoja na Balozi wa Cuba
nchini Tanzania Mhe.Jorge Luis Lopez Tormo wakimkabidhi Rais Dkt.Jakaya
Mrisho Kikwete picha ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere akiwa na
Rais kiongozi wa Taifa la Cuba Fidel Castro wakati wa uwekaji jiwe la
msingi kiwanda cha Viuadudu vya kuua viluwiluwi vya mbu wanaoeneza
Malaria katika hafla iliyofanyika Kibaha mkoani Pwani leo.Wapili kushoto
ni Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt.Abdallah Kigoda.Mradi huo
utaendeshwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Tanzania na serikali ya
watu wa Cuba.
Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu




No comments:
Post a Comment