Header Ads

WANAFUNZI UDOM WAPATA KIWEWE BAADA YA BODI YA MIKOPO KUTOA MAJINA YALIYO NA KASORO NA MWISHO WA KUSAJILI UPYA NI LEO

Baadhi ya Wanafunzi Wa UDOM wakirudia kujisajili huku wengine wakiangalia majina yao kwenye tovuta ya bodi ya mikopo kuona kama majina yao ya makosa.Wale ambao majina yao ya kasoro wametakiwa kujaza tena na kutuma upya huku ikiwa mwisho ni leo na baadhi ya majina yakiwa hayajatoka.
Wanafunzi Wa Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) wakiwa bize sana kujisajili kusajili masomo yao ya muhula wa kwanza kupitia mtandao wa intaneti na wengine wakirudia kujisajili tena kupitia intaneti kwaajili ya kupewa mkopo baada ya majina yao kurudishwa yakiwa na kasoro .Wanafunzi Hao wakionekana kuchoka kutokana na kasi ya intaneti kuwa chini na kuleta usumbufu
Kama Wanavyooneka wanafunzi wakiwa bize kusajili masomo yao huku wengine wakiangalia majina yaliyotolewa ya wanafunzi ambao majina yao yana kasoro na kutakiwa kurudia kujazwa upya na kutumwa tena kupitia mtandao wa kompyuta huku mwisho wa kufanya hivyo ni leo tarehe 26/10/2011 wakati kuna majina mengine yanaendelea kutolewa na bodi ya mikopo kupitia tovuti yao.

No comments:

Powered by Blogger.