Header Ads

JK, MAMA SALMA KATIKA MKUTANO WA JUMUIYA YA MADOLA

Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Mwenyekiti wa watanzania waishio Australia, Asimwe Kabunga katika mkutano unaowajumuisha watanzania waishio Australia. Rais Kikwete pamoja wanajumuia ya watanzania wanaoishi Australia wamezungumzia masuala mbalimbali ya maendeleo. (PICHA ZOTE NA MWANAKOMBO JUMAA-MAELEZO)
Baadhi ya wanajumuia wanaoishi nchini Australia wakimsikiliza Rais Jakaya Kikwete (hayupo pichani) alipokutana nao nchini Perth.
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete akibadilisha mawazo na mwanajumuia wa kitanzania aishie Australia, Dk. Joseph Masika wakati Rais Jakaya Kikwete alipokutana na wanajumuia hao wanaoishi Australia na kuzungumza nao mambo mbalimbali ya maendeleo ya nchi yetu.

Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete (kulia) akipokea maua kutoka kwa mweka Hazina wa Jumuia ya Watanzania waishio Australia, Maryam Powell, walipokutana na wanajumuia mjini Perth Australia. Rais Jakaya Kikwete alikutana na wanajumuia kuzungumza mambo mbalimbali ya maendeleo na kijamii. Rais yupo nchini Australia kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi wanachama wa Jumuia ya Madola.
Wanajumuia wa kike wanaoishi Australia wakiwa katika picha ya pamoja na Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete baada ya kumalizika mkutano wa Rais Kikwete na Watanzania wanaoishi Australia jana.

No comments:

Powered by Blogger.