PUSH OBSEVER YAZINDULIWA ASUBUHI YA JANA KEMPISKI HOTEL
Mdau wa akiendelea na kumwaga habari na maelezo zidi juu ya hiyo kampuni mpya ...
Ufuatiliaji wa matangazo kwenye
redio
na televisheni ulikuwa mgumu kutokana na kukosekana teknolojia ya
kisasa ya kufuatilia, watangazaji wakubwa nchini, kama vile makampuni ya
simu na vinywaji baridi, wakati mwingine walikuwa wanalipa hata
matangazo ambayo hayakurushwa. Lakini kwa ujio wa kampuni ya Push
Observer, tatizo hilo litabaki historia. Kwa kutumia teknolojia ya
kisasa, mtangazaji hivi sasa ataweza kufuatilia na kupata repoti ya
ambavyo matangazo yake yalirushwa redioni au kwenye televisheni, kwa
kuangalia sekunde, dakika, siku na mara ngapi lilirushwa tangazo hilo.
Mpango mzima wa uzinduzi umefanyika asubuhi hii Kempinsky Hotel, jijini
Dar es salaam. Pichani juu ni Ofisa Mkuu wa Operesheni wa kampuni ya
hiyo, Omary Salisbury akielezea namna teknolojia hiyo inavyofanya kazi.
Kwa Habari Zaidi <<< BOFYA HAPA >>>
No comments:
Post a Comment