Header Ads



USIMAMIZI WA RASILIMALI ZA NCHI HII YA TANZANIA

            Rasilimali ni vyanzo vya nchi ambavyo  vinasaidia nchi kiuchumi ni zawadi tuliyopewa na Mungu kama urith wa dunia.Nchi hii ya Tanzania tunazo rasilimali nyingi ambazo ni; maadini, mbuga za wanyama, milima ,mito, maziwa, bahari na vinginevyo vingi.Lakini tumeona rasilimali nyingi za nchi hii zikitumiwa na wajanja wachache ambao hawalitakii mema taifa hili tungeona kama zingetumiwa vizuri nchi ingefaidika na uchumi ungekuwa.

            Sekta ya madini: Madini ni rasilimali nzuri sana kama itatumiwa vizuri itanufaisha watanzania kwani Tanzania tunayo madini ya aina nyingi kama; dhahabu alimasi, makaa ya mawe na tanzanite ambayo inapatikana Tanzania pekee duniani.Tumeona serikali imeshindwa kusimamia vizuri sekta hii ambayao itasaidia nchi kupiga hatua,Naishauri serikali kuchunguza sekta hii kwani imejaa rushwa ufisadi mkubwa ambao unasababisha nchi kuwa masikini kwa ajili ya watu wachache ambao hawaitakii Tanzania mema.Madini ndiyo rasilimali ndiyo  tuliyopewa na Mungu kama zawadi ya kututoa kwenye shida.

            Mbuga za Wanyama; Tumeona mbuga mbuga zetu za wanyama kama Ngorongoro, Manyara,Serengeti Mikumi pamoja na nyingine ambazo ni ndogo zipo ndani ya nchi hii ni rasilimali ambazo huingizia serikali mapato mengi kwa utalii na kusaidia uchumi kukua. Lakini tumeona sekta hii imekuwa na ubadhilifu mkubwa wa Ruswa na Ufiksadi na kuiacha nchi ikiwa masikini.Wanyama wanatorooshwa na kuuzwa nje pamoja na uwindaji holela ambao unafanywa na baadhi ya wananchi kwa kushirikiana na viongozi ambao wanahusika na sekta hii.Naiomba serikali yangu ichunguze hawa watu wachache wanaohujumu uchumi wa nchi kwa kuiibia serikali katika rasilimali hii ya utalii ambayo inaingizia serikali fedha nyingi ambazo zinasaidia uchumi kukua.

            Milima yetu; Milima ni mojawapo ya railimali ambazo hutuingizia fedha za kigeni  kwa Utalii ambazo zinasaidia Taifa kusonga mbele kwa kuua uchumi.Fedha hizi kama zinatumika vizuri zitasaidia kukuza uchumi  wa Taifa  la Tanzania. Kuondokana na umasikini,mlima Kilimanjaro meru na uluguru ni rasilimali  za kujivunia kwa husaidia nchi ambayo ni changa kama Tanzania kujikwamua kwenye dibwi hili la umaskini  naomba serikali hii isaidie kusimamia fedha hizi zinazopatikana kutokana na rasilimali hizi ambazo ni za wale tulopewa mungu kama uridhi wan chi yetu ya Tanzania

Bahari yetu ya hindi hii ni moja wpo ya rasilimali tuliyopewa na mungu kama zawadi kutoka kwa mungu lakini haitumiwi vizuri na watanzania kwa kuchafua bahari na kutumia mabomu kuangamiza viumbe waliopo ndani ya maji kama samaki dagaa pamoja na aina zote za wanyama waliopo ndani ya bahari naiomba serikali isimamie vizuri Bahari yetu ya hindi na kukomesha wavuvi haramu ambao halitakii taifa mema . Nchi inaweza uza samaki na dagaa na kusaidia kukuza uchumi wa Taifa hili Pia Bahari yetu ni Moja wapo ya Utalii wa kujitangaza  kimataifa 

Maziwa yetu: Maziwa yetu ndani ya nchi hii ni muhimiu sana kama rasilimali ya nchi tumeona kuna ziwa kama Victoria ambalo maporomoko yake husaidia katika swala la umeme Pamoja na kutupatia samaki .
Gesi: Hii ni moja wapo ya rasili mali ya Taifa hili ambayo inasaidia nchi kukua kiuchumi na kuwasaidia watanzania kupata Nishati ambayo itawasaidia katika maswala yao ya kila siku Naishauri serikali kusimamia vizuri rasilimali hii ya gesi ambayo inaingizia Taifa Hela Nyingi na kuinua Pato la Taifa kukua na Kuondolea watanzania Umaskini uliotanda ndani ya macho ya watanzania Serikali isikubali watu wachache watumie rasilimali hii muhimu kujinufaisha wenyewe kwa kutumia nishati kama rasilimali ya wachache .

Makaa ya mawe: Nishati hii ni muhimu kwa kulisaidia Taifa kiuchumi kwa kuongeza pato la Taifa naishauri serikali kusimamia nishati hii muhimu na kuanza kuchimba ili iweze kuwanufaisha watanzania kama itakuwa haiwanufaishi watanzania Haina haja ya kuchimbwa kwani itakuwa imewanufaisha wachache Nishati hii ni muhimu kwani nchi inabaki maskini huku ikiwepo Rasilimali Muhimu kama hii.


Sehemu ya Kitalii Zanzibar na Bagamoyo : Hii nimoja wapo ya rasilimali inayotupatia fedha za kigeni kwa kuangalia mambo ya kale yaliyofanywa na babu zetu. Na kutuachia ukumbusho wa vitu ambavyo ni vya kukumbukwa na kuenziwa kama fahari ya nchi na rasilimali ya kujivunia . Naishauri serikali kuwa makini kwa sekta hii imejaa rushwa na kulikosesha Taifa fedha za Kigeni watalii wanaingiza fedha nyingi Lakini hazionekani kwani zinaishia kwa wajanja wachache Kama sekta hii itazibitiwa vizuri basi Taifa Litakuwa linanufaika na Rasilimali hii muhimu tuliachiwa na Babu zetu kwa manufaa ya vizazi vijavyo.

Mapango ya mboni Tanga:  Hii nayo ni moja wapo ya rasilimali ya nchi kwani nayo hutupatia fedha za kigeni kama sehemu ya kitalii kwa maajabu ya mapango ya mboni Tanga tunaona serikali inapata fedha nyingi kwa kivutio hiki ambacho husaidia kukuza uchumi wa Taifa letu lakini kama hakutakuwa na usimamizi mzuri wa fedha inayopatika wananchi watakuwa hawanufaiki na rasilimali hii ambacho ni kivutio cha wageni na watu wa ndani kama sehemu ya uchumi wan chi.


Bonde la oldivai George: Hii ni moja wapo ya uridhi tulioupata kwa babu zetu kama Historia ya nchi Tunajua Oldivai George ni  bonde lililopatikana fuvu la binadamu wa kwanza kuishi liligunduliwa huko arusha mwaka 1958 na Kuwekwa kwenye historia ya nchi kama sehemu ya kitalii . Taifa limekuwa likipata fedha kwa kivutio hiki ambacho kimekuwa kikisaidia kuinua uchumi wan chi. Naomba serikali yangu iwe inasimamia vizuri mapato yanayopatikana kwani kufanya hivyo itawanufaisha umma kunufaika na rasilimali za nchi hii.

Nimeona nizungumzie kuhusu usimamizi wa rasilimali za nchi hii ya Tanzania . Kwani ndio moyo wa wananchi na si rasilimali za viongozi wa umma peke yake nchi hii kumekuwa na tabia moja ya rasilimali kufaidika na viongozi na kuacha watanzania wakiishi maisha ya kimaskini huku migodi ikibaki mashimo tu. Na kinachopataikana hakijulikani kinaenda wapi tumeona wanyama wetu wakiuzwa kinyemela kwa ujanja wa wachache huku watanzania wakikosa rasilimali za nchi yao . Namuomba Mh. Jakaya Mrisho Kikwete Kufuatilia swala hili la usimamizi wa rasilimali za watanzania na kuhakikisha zinawanufaisha wananchi na si vigogo wachache wenye kukosa utu na uruma kwa watanzania namsihi atoe adhabu kali kwa wale wanaopatikana na makosa ya kuhujumu rasilimali za nchi hii na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria akijaribu kuchukua hatua basi Taifa litasonga mbele na uchumi wa Taifa hili utakuwa na Kustawi kwani wanaotusababishia umaskini ndani ya Taifa hili ni wajanja wachache ambao wamekuwa sumu ndani ya nchi hii kwa kujinufaisha na rasilimali za watanzania.

Mwisho nawasihi watanzania Wakati umefika wakujua kilicho chao na kuambia Mafisadi, wala rushwa basi imetosha tumechoshwa na kutunyonya kwa kutumia rasilimali zetu kwa maslahi yao binafsi.

Ni mimi Mpenda Maendeleo:

DENIS BAHATI HENRY
Mungu ibariki Tanzania
Mungu Ibariki Afrika.
0712 550508
0765 002472 



TUNDU LISSU DHAMANA YAMTOA  JELA 

Kiongozi huyu asema jela panatisha,aomba haki za binadamu zifuatwe....

Mbunge wa Singida Mashariki kupitia CHADEMA, Tundu Lissu na wenzie saba wameachiwa kwa dhamana ya sh. milioni 70 na kuambiwa wasifike eneo la Nyamongo, Tarime ambapo yalitokea mauaji ya watu kadhaa. Watu hao wameshitakiwa kwa makosa matatu yakiwamo ya kuvamia Hospitali ya Wilaya ya Tarime kulimokuwa kumehifadhiwa maiti, na kufanya kusanyiko pasipo halali.

No comments:

Powered by Blogger.