NDOA YA ARNOLD SCHWAZNIGGER KUVUNJIKA.
Sababu ni mtoto wa nje aliyezaa na
mfanyakazi wa nyumbani kwake miaka 10 iliyopita.Mwanamke anaitwa
Mildread Baena walifanya mapenzi na Shwaznigger nyumbani kwenye nyumba
anayoishi na familia yake.Hata wakati wa ujauzito bibie aliendelea
kufanya kazi katika nyumba hiyo.
Kweli moyo wa mtu ni kichaka,jamaa
alikaa kimya miaka yote hiyo mpaka hii majuzi alipomueleza
mkewe.Wadadisi wa mambo wanasema ndio sababu zilizopelekea ndoa yake ya
miaka 25 na mkewe Maria Shriver kuvunjika.Tarehe 9 mwezi huu wanandoa
hao walitangaza kutengana na tarehe 17 Shwaznigger akaomba msamaha kwa
kuwa na mtoto na mwanamke huyo aliyekuwa mfanyakazi nyumbani kwao.
Reviewed by
crispaseve
on
3:46 PM
Rating:
5
No comments:
Post a Comment