Header Ads

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalimakutana na mgombea uenyekiti wa IPCC na Balozi wa Comoro nchini Inbox

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akizungumza na Mgombea wa nafasi ya Uenyekiti kwenye Kundi la Wataalam chini ya Umoja wa Mataifa linaloshirikisha wadau kutoka sekta ya umma na binafsi kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi-Intergovernmental Panel on Climate Change-IPCC, Prof. Jean-Pascal Van Ypersele kutoka Ubelgiji ambaye alifika Wizarani kwa ajili ya kumsalimia Mhe. Maalim. Katika mazungumzo yao Prof. Ypersele alielezea dhamira yake ya kushirikiana na nchi zinazoendelea katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa kuongeza wataalam kwenye kundi hilo pindi atakapochaguliwa kwenye nafasi hiyo.
Prof. Ypersele nae akichangia jambo wakati wa mazungumzo yao. Kushoto ni Balozi wa Ubelgiji hapa nchini, Mhe. Koenraad.
Mazungumzo yakiendelea
Balozi Adam akisaini Kitabu cha Wageni Ofisini kwa Mhe. Mahadhi
Prof. Ypersele nae akisaini Kitabu cha Wageni

No comments:

Powered by Blogger.