Header Ads

YANGA KISICHO RIZKI HAKILIKI …yabanwa nyumbani na Ndanda FC

Ikicheza nyumbani, Yanga ya Dar es Salaam imelazimishwa sare ya bila kufungana na Ndanda FC ya Mtwara katika mchezo wa Ligi Kuu uliochezwa Uwanja wa Taifa.
Yanga ilitengeneza nafasi nyingi za kufunga lakini washambuliaji wake walikosa umakini wa kuchomeka mipira wa wavuni.
Nafasi ya wazi zaidi kupotezwa na Yanga ilikuja dakika ya 77 wakati Amis Tambwe alipomimina krosi ya chinichini kutoka upande wa kulia na mpira ukamkuta Danny Mrwanda akiwa yeye na wavu lakini kwa mshangao wa wengi akapaisha mpira juu.

No comments:

Powered by Blogger.