Header Ads

THIERRY HENRY ASEMA CHELSEA ITATWAA UBINGWA ENGLAND … amvulia kofia Jose Mourinho

Chelsea players celebrate at the corner flag after the France international breaks the first half deadlock
Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal na Barcelona Thierry Henry amesema anaamini Chelsea itatwaa ubingwa wa Premier League kwa sababu Jose Mourinho anajua namna ya kupata matokeo mazuri hata pale timu yake inapocheza vibaya.
Thierry Henry aliyekuwa mchambuzi wa mechi ya Chelsea dhidi ya mabingwa watetezi Manchester City katika dimba la Stamford Bridge, anasema Mourinho anatakiwa ajihesabu kuwa ni mwenye bahati kwa kuepuka kipigo na kuambulia pointi moja.
Katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya 1-1, City ilicheza vizuri zaidi na kutengeneza nafasi nyingi za magoli ingawa umaliziaji ulikuwa tatizo.
Chelsea ilikuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwa Loic Remy lakini wakawa chini ya shinikizo kubwa baada ya David Silva kusawazisha na kufuatia hali hiyo Thierry anasema klabu hiyo ya London imeonyesha alama zote za kuwa mabingwa wapya wa Premier League.
“Tunastahili kuwapa pongezi Manchester City kwa kuchukua pointi moja ‘darajani’? Hapana,” alisema Henry kupitia Sky Sports baada ya mchezo huo.
“Walisawazisha, wakamiliki sana mpira pamoja na kuwa na nafasi nyingi zaidi za kufunga. Hawakushinda.

“Hivyo  ndivyo wanavofanya Chelsea. Wakati fulani wanaweza wasicheze vizuri lakini wakashinda 1-0. Wamehangaika sana leo (jana) lakini hawakupoteza mchezo. Hii ndio sababu inayonifanya niamini kuwa Chelsea itatwaa ubingwa.”

No comments:

Powered by Blogger.