WAKUTANA KUJADILI MKAKATI WA MRADI WA KIJIJI CHA DIGITALI
Ofisa
Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la
Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph,
akiwasilisha mada ya mchanganuo wa ufumbi wa changamoto mbalimbali
katika utekelezaji wa mradi wa kijiji cha kidigitali.
Na Mwandishi wetu, Bagamoyo
WADAU
mbalimbali wa elimu, afya, Tehama na masuala ya utamaduni na uchumi
ambao wamo katika mradi wa kijiji cha dijiti cha Ololosokwan kilichopo
wilayani Monduli Arusha wanakutana kwa warsha ya wiki moja ikiwa ni
sehemu ya mandalizi ya uwapo wa kijiji hicho nchini Tanzania.
Kwa
mujibu wa Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la
Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini Al Amin Yusuph
warsha hiyo imelenga kuangalia changamoto na namna ya kuzitatua ili
mradi kuwa na tija kwa wananchi wake.
Yusuph
alisema kwamba wadau hao wanapanga mkakati kuangalia vipaumbele na
changamoto katika utekelezaji wa mradi huo wa miaka mitatu.
Alisisitiza
kwamba kwa kuwa mradi huo utakuwa na mawasiliano ya kisasa, masomo kwa
njia ya Tehama, tiba kwa kutumia mtandao wadau wamekusanyika mjini
Bagamoyo kuangalia namna bora ya kuufanya mradi huo uwe endelevu hata
kama UNESCO na mbia wake Samsung watajiondoa huko mbeleni.
No comments:
Post a Comment