Header Ads

RIDHIWANI KIKWETE AAPA KUPAMBANA NA MATAPELI WA ARDHI JIMBO LA CHALINZE

 Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete,akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Fukayosi, Kata ya Fukayosi, wakati wa ziara ya kikazi pamoja na kuwashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa mbunge miezi  sita iliyopita.Ridhiwani kutoruhusu hata kipande cha heka moja kuporwa na matapeli katika jimbo lake la Chalinze.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Kijana Salumu Khamis akiuliza swali mbele ya Mbunge Ridhiwani Kikwete kuhusu tatizo la maji katika Kijiji cha Fukayosi
 Mkuu wa Miradi wa Mkoa wa Pwani wa Tanesco, Leo Mwakatobe, akielezea jinsi umeme utakavyosambazwa katika Kijiji cha Fukayosi na vijiji vingine Jimbo la Chalinze.
 Mwenyekiti mpya wa Serikali ya Kijiji cha Fukayosi, Salum Mkwecha akimshukuru mbunge kwa ahadi mbalimbali alizozitoa katika miradi mbalimbali katika kijiji hicho.
 Ridhiwani akibadilishana mawazo na mmoja wa watawa baada ya kumalizika kwa mkutano katika Kijiji cha Fukayosi Jimbo la Chalinze.
 Mwenyekiti mstaafu wa Kata ya Fukayosi,Adam Masoud  akimuomba Mbunge Ridhiwani kuhikisha anaweka miundombinu ya barabara na maji na masuala ya afya katika Kijiji cha Mkenge,wakati wa ziara yake katika Kata ya Fukayosi ya kuwashukuru kwa kumchagua pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kuangalia jinsi ya kuzitafutia ufumbuzi.

No comments:

Powered by Blogger.