Mabingwa wa Soka Tanzania Azam Fc Kuweka Kambi Nchini Kongo

Mabingwa
wa Soka nchini Tanzania Azam Fc wanatarajia Kuweka kambi nchini Jamhuri
ya Kidemokrasia ya Kongo kwaajili ya kucheza mechi nne za kirafiki
ikiwa ni kujiandaa na mechi ya ligi ya klabu bingwa ya Afrika dhidi ya
vigogo wa Sudan timu ya El-Merreikh
Jaffar
Iddi, msemaji wa klabu ya Azam amesema wakiwa Congo, watacheza na timu
kubwa nne na kurejea nchini Tanzania Mnamo February 4 kwaajili ya
kujiandaa na kucheza Mechi na Elh-Merreikh Jijini Dar kati ya February
13, 14 na 15.
“Bado hatujajua timu tutakazocheza nazo kwa kuwa bado tupo katika mazungumzo aliongezea Jaffar”.
Ni
mara ya kwanza kwa timu ya Azam kushiriki ligi ya klabu bingwa Afrika,
Azam Fc inatarajia kuondoka kuelekea Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya
Kongo mara baada ya kumaliza kucheza mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara
ambayo itachezwa January 24 dhidi ya mabingwa wa zamani Wekundu wa
Msimbazi Simba Sports Club.
Wakati
Azam wakiwa kwenye maandalizi ya Mechi yao wapinzani wao El-Merreikh
tayari washacheza mechi kadhaa za majaribio ikiwa pamoja na kutoka sare
ya magoli 2 kwa 2 na Timu ya Schalke 04 inayoshiriki ligi ya Bundersliga
nchini Ujerumani.
Mbali
na Azam, wawakilishi wengine wa Tanzania katika michuano ya CAF ya
vilabu ni Young Africans (Yanga), wanaotegemewa kucheza na timu ya jeshi
la Botswna, BDF XI katika mechi ya awali ya kombe la shirikisho.
Kwa
upande wa Zanzibar, mabingwa KMKM watakiputa na timu nyingine ngumu ya
Sudan, Al Hilal katika klabu bingwa Afrika wakati katika kombe la
shirikisho, Polisi watacheza na CF Mounana ya Gabon.
No comments:
Post a Comment