Vijiji 45 mkoani Mara kupatiwa umeme
Profesa Muhongo aliyasema hayo katika ziara yake ya siku sita
katika mkoa wa Mara lengo likiwa ni kukagua na kuzindua miradi ya umeme
vijijini inayosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) awamu ya pili
kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Nchini (Tanesco).
Profesa Muhongo alisema ziara yake iliyohusisha wilaya za Musoma
Vijijini, Tarime, Rorya, Bunda na Serengeti ililenga pia kubaini na
kukagua mahitaji ya umeme katika wilaya hizo ili vijiji vilivyokosa
umeme kwenye awamu ya pili viingizwe katika awamu nyingine ya umeme
vijijini.
Alieleza kuwa Wizara imekuwa ikisambaza umeme katika kila Mkoa
na Wilaya za Tanzania kwa awamu kulingana na mahitaji na idadi ya watu
katika maeneo hayo.
Alisema kwa sasa umeme unaosambazwa upo katika awamu ya pili ambapo awamu ya tatu itakuja baada awamu ya pili kumalizika. Alisema vipaumbele vinavyotolewa katika uunganishaji wa umeme
vijijini Profesa Muhongo alitaja kuwa ni maeneo yenye huduma muhimu za
kijamii kama vile mashule, vituo vya afya, makanisa, misikiti, ofisi za
vijiji na kata, na sehemu zenye miradi ya maji.
No comments:
Post a Comment