Header Ads

UTURUKI NA TANZANIA YASAINI MAKUBALIANO YA AWALI (MoU) KATIKA UIMARISHAJI WA SEKTA YA MADINI

 Mtendaji Mkuu wa  Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) Profesa Abdulkarim Mruma (kushoto waliokaa) na Naibu Mkurugenzi Mkuu  wa  Kurugenzi ya Utafiti wa Madini ya  Uturuki Dkt. Abdulkerim Yorukoglu ( kulia waliokaa) wakisaini makubaliano ya  awali (MoU) kwa ajili ya ushirikiano wa taasisi hizo katika masuala ya  utafutaji wa madini na ubadilishanaji  wa ujuzi, uzoefu na teknolojia.  Waliosimama kushoto ni Kamishna Msaidizi  wa Madini, Ukaguzi wa Migodi  Mhandisi Ali Samaje na kulia ni  Balozi wa Uturuki Nchini, Ally Davutoglu.
 Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akisisitiza jambo  kwenye ufunguzi  wa kikao kwa ajili ya kusaini  makubaliano ya awali (MoU) kati ya  Kurugenzi ya Utafiti wa Madini ya  Uturuki na Wakala wa Jiolojia  Tanzania  (GST)

 Mtendaji Mkuu wa  Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) Profesa Abdulkarim Mruma akielezea  majukumu ya wakala huo katika kikao hicho.
Kamishna Msaidizi  wa Madini, Ukaguzi wa Migodi  Mhandisi Ali Samaje akielezea aina  za madini  yanayopatikana nchini Tanzania katika kikao hicho.

No comments:

Powered by Blogger.