WIZARA YA BISHARA ZANZIBAR YAPATA MSAADA KUTOKA WIZARA YA BIASHARA (SMT)
……………………………………………………………………………………
Na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar
Wizara ya Biashara na Viwanda ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekabidhi Gari na Vifaa vya Ofisini kwa
Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko ya Zanzibar katika hafla
iliyofanyika leo Wizarani Malindi mjini Unguja.
Msaada huo uliofadhiliwa na Shirika
la Biashara la Dunia WTO ulitolewa ili kuijengea uwezo Wizara ya
Biashara ya Zanzibar katika kukabiliana na majukumu yake ya kila siku.
Akikabidhi Msaada huo Mkurugenzi
Sera na Mipango wa Wizara ya Biashara ya Bara Edward Sungula kwa Katibu
Mkuu wa Wizara ya Biashara ya Zanzibar Julian Raphael amesema Suala la
Biashara ya Kimataifa ni la Muungano hivyo Serikali mbili lazima
zishirikiane na kusaidiana katika kutekeleza majukumu yao.
Amesema Msaada huo ni utekelezaji
wa Mradi wa “Capacity Building for Trade Development and Integration
Project” ambao una lengo la kuzijengea uwezo Serikali katika kutekeleza
misaada chini ya utaratibu wa “AID FOR TRADE”.
Ameongeza kuwa msaada huo ni mwanzo wa kudumisha ushirikiano katika kutekeleza mradi huo na njia ya kuendeleza kudumisha Muungano uliopo baina ya Tanzania Bara na Zanzibar. Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Masoko Zanzibar Julian Raphael ameishukuru Wizara hiyo juu ya Msaada huo na kuongeza kuwa utachochea ufanisi katika majukumu yao. Katika kutekeleza Mradi huo wa kukuza Sekta ya Biashara Tanzania Bara na Zanzibar Mradi umeanza kwa kununua Vifaa ambavyo ni pamoja na Gari mbili, Komputa, Projekta na Mashine ya Kuprintia.
Ameongeza kuwa msaada huo ni mwanzo wa kudumisha ushirikiano katika kutekeleza mradi huo na njia ya kuendeleza kudumisha Muungano uliopo baina ya Tanzania Bara na Zanzibar. Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Biashara na Masoko Zanzibar Julian Raphael ameishukuru Wizara hiyo juu ya Msaada huo na kuongeza kuwa utachochea ufanisi katika majukumu yao. Katika kutekeleza Mradi huo wa kukuza Sekta ya Biashara Tanzania Bara na Zanzibar Mradi umeanza kwa kununua Vifaa ambavyo ni pamoja na Gari mbili, Komputa, Projekta na Mashine ya Kuprintia.
No comments:
Post a Comment