Header Ads

NMB YATOA MAFUNZO KWA WAJASIRIAMALI JIJINI DAR ES SALAAM





 Mtoa mada kuhusu kodi kutoka kampuni ya ‘Tanscott Taxation Service Ltd’ Bw. Hirji Abdallah akielezea kuhusu ulipaji wa kodi wakati wa semina ya wajasiriamali iliyondaliwa na benki ya NMB .Semina hiyo ulihudhuriwa na wanachama zaidi ya 400 wa NMB Business Club kutoka Wilaya ya Kinondoni, Ilala na Temeke hivi karibuni jijini Dar es salaam.
Meneja wa NMB anayeshugulikia Mikopo Midogo Midogo Mashaga Changarawe akiongea na wateja wa NMB katika semina hiyo ya wajasiriamali iliyoandaliwa na benki ya NMB.
Mwanachama wa NMB Business Club Wilaya ya Temeke Bibi Pili Matimbwa akichangia mada wakati wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa NMB Business Club Wilaya ya Kinondoni Bw. Ramadhani Njiku akielezea mafanikio waliyoyapata wanachama wa  NMB Business Club Wilaya ya Kinondoni  tangu kuanzishwa kwake.
Mwenyekiti wa NMB Business Club Wilaya ya Ilala Bw. Henri Ignas Mrema akielezea jinsi  wana NMB Business Club Kanda ya Kinondoni  walivyonufaika na klabu hiyo tangu kuanzishwa  kwake na wanavyoendelea  kufurahia huduma na bidhaa kutoka benki ya NMB. Akitoa shukurani kwa niaba ya wanachama wake kwa uongozi wa benki ya NMB kwa kuandaa semina ambazo zinatoa mafunzo yanayowajenga wanachama wa NMB Business Club.
Mwenyekiti wa NMB Business Club Kanda ya Temeke Bw. Ezekiel Matimo Gutti akiongea  machache  kuhusu  NMB Business Club Wilaya  ya Temeke  tangu kuanzishwa  kwake.

No comments:

Powered by Blogger.