Header Ads

Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imetangaza bei mpya za umeme ambazo zimepanda kwa kuzingatia makundi tofauti ambayo ni..

Mkurugenzi wa Uchumi Mdhibiti wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), Felix Ngamlagosi akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, alipokuwa akitangaza viwango vipya vya bei ya umeme. Kulia ni Mkurugenzi wa Umeme wa mamlaka hiyo, Anastas Mbawala. Picha na Silvan Kiwale  
---
 Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) imetangaza bei mpya za umeme ambazo zimepanda kwa kuzingatia makundi tofauti.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkurugenzi Mdhibiti Uchumi wa Ewura, Felix Ngamlagosi alisema bei mpya zitaanza kutumika Januari Mosi, 2014 mpaka Desemba 2016. Hata hivyo, alisema mabadiliko ya bei yanaweza kutokea katikati ya kipindi hicho cha miaka mitatu.
Bei mpya ya umeme
Ngamlagosi alisema mwananchi wa kipato cha chini anayetumia uniti (0-75) kwa mwezi, atalazimika kulipia Sh100 kwa uniti ukilinganisha na Sh60 iliyokuwapo awali.
Ongezeko lipo pia katika kundi linaoitwa T1 la watumiaji wakubwa wa umeme wa nyumbani, ambao watalipia Sh306 kwa uniti ikiwa ni ongezeko la Sh85 ya bei iliyopo sasa.
Alisema katika kundi la T2 la wateja wakubwa wanaopimwa kwenye matumizi ya uniti 7,500, malipo ya uniti moja yamefikia Sh205 ikiwa ni ongezeko la Sh73 kutoka bei ya sasa.
 
“Kundi jingine la T3-MV ambao ni wateja wa viwanda vikubwa, litaanza kulipia Sh166 kwa uniti ikiwa ni ongezeko la Sh45 ya bei ya sasa pamoja na kundi la T3HV lililounganishwa kuanzia voti 66,000 na zaidi ambalo litaanza kulipia Sh159 kwa uniti ikiwa ni ongezeko la Sh53,” alisema Ngamlagosi.

No comments:

Powered by Blogger.