Tume ya Mabadiliko ya Katiba yaendelea na Awamu ya Nne ya kukusanya maoni
Mikoa hiyo ni Dar es Salaam,
Arusha, Simiyu, Geita, Mara na Mjini Magharibi na kila siku kutafanyika
mikutano miwili, wa kwanza utaanza saa 3:00 asubuhi – saa 6:00 mchana na
kufuatia na mwingine utakaoanza saa 8:00 alasiri – saa 11:00 jioni.
Taratibu zote za kuanza kazi ya
kukusanya maoni katika mikoa iliyotajwa zimekamilika zikiwemo kuandaa
ratiba na kuisambaza katika ofisi za mikoa, wilaya na Halmashauri za
Manispaa na Wilaya husika. Wajumbe wa Tume na watumishi wa Sekretarieti
wamejigawa katika makundi saba. Kila mkoa utakuwa na kundi moja
isipokuwa Dar es Salaam ambao utakuwa na makundi mawili.
No comments:
Post a Comment