Meneja
wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), mkoa wa Katavi Eng. Abdon
Maregesi akimuonesha athari za mvua Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia kwake) wakati akikagua daraja
la Koga lililoathirika. Daraja hilo linaunganisha mkoa wa Katavi na
Tabora.
Muonekano
wa Daraja la Koga baada ya kufanyiwa ukarabati kufuatia kuathiriwa na
mvua kubwa zilizonyesha katika mkoa wa Katavi. Daraja hilo kwa sasa
linaruhusu magari kupita ya tani 1 hadi 3.
Muonekano
wa barabara ya Tabora-Koga-Mpanda yenye urefu wa Km 356 inayojengwa kwa
kiwango cha lami ikiwa katika hatua za awali za ujenzi wake.
Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa
maelekezo kwa mkandarasi wa kampuni ya CICO anayejenga barabara ya
Tabora-Koga- Mpanda yenye urefu wa Km 356, sehemu ya Tabora-Sikonge
kumaliza mradi huo kwa wakati.
Mkuu
wa Wilaya ya Sikonge Bi. Hanifa Sirengu akitoa taarifa kwa Waziri wa
Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kuhusu hali ya
miundombinu katika wilaya yake.
WAZIRI PROF. MBARAWA AKAGUA BARABARA YA TABORA-KOGA-MPANDA KM 356
Reviewed by
crispaseve
on
1:36 AM
Rating:
5
No comments:
Post a Comment