Header Ads

UMEME WA GESI ASILIA KUANZA KUTUMIKA HIVI KARIBUNI

 Waziri wa nishati na madini George Simbachawene akiwa na wajumbe wa Tanesco akitembelea miradi ya umeme wa gesi alisilia iliyogunduliwa Mtwala, katika kituo lilichojengwa na Kampuni ya mafuta ya Tanzania Petrolium Development Corpolation (TPDC) hii ni sehemu iliyojengwa ni kituo kikubwa cha kutunzia gesi ya kutengenezea umeme katika kituo cha Kinyerezi jijini Dar es Salaam leo.
 Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Dk.James Mataragio akizungumza na waandishi wa habari katika katika ziara ya waziri wa nishati na madini George Simbachawene, kukagua miradi ya umeme wa gesi asilia katika kituo kikubwa cha kufikia gesi asilia kilichopo kinyerezi jijini Dar es Salaam leo.
 Waziri wa Nishati na Madini,George Simbachawene akizungumza na waandishi wa habari leo katika kituo cha kufikia gesi asilia inayotoka Mtwala ili iweze kutengeneza umeme kutokana na umeme wa maji kupungua kutokana na vyanzo vya maji vya mto Mtera na Kihansi kupungua maji kwaajili ya mabadiliko ya hali ya hewa.Kushoto ni Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Dk.James Mataragio.
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene akiwa na Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Dk.James Mataragio. wakielekea kwenye kituo cha kutengeneza umeme cha Tanesco kilichopo Kinyerezi jijini Dar es Salaam baada ya kukagua kituo cha gesi hii leo katika ziara ya kukagua miradi hiyo.

Picha na Avila Kakingo,Globu ya Jamii.

No comments:

Powered by Blogger.