TUME YA HAKI ZA BINADAMU, UNESCO WATAKA JAMII KUTAMBUA WATU WENYE ALBINISM
Kamishna
wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Dkt. Kevin Lothal Mandopi
akielezea namna ya tume hiyo ilivyo mstari wa mbele kuelimisha Umma
dhidi ya vitendo na ukatili kwa watu wenye Ualbinism nchini kwa wadau na
waandishi wa habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam mapema leo
Juni 13.2015.
Na Andrew Chale, modewjiblog
Tume
ya Haki za binadamu na Utawala bora nchini, leo Juni 13,2015,
imeungana na watanzania wote kuadhimisha siku ya Kimataifa ya
uelimishaji umma kuhusu Ualbino na haki za watu wenye Ualbino ambapo
imeitaka jamii kutambua haki na wajibu wa kuwalinda na kuwathamini.
Akisoma
taarifa maalum kwa wadau mblimbali na waandishi wa habari
waliojitokeza jijini Dar Es Salaam, Kamishna wa tume hiyo, Dkt. Kevin
Lothal Mandopi alieleza kuwa jamii inayo wajibu wa kuwathamini watu hao
wenye albinism kwani nao ni kama binadamu wengine na wana haki sawa.
Kamishna
Mandopi katika taarifa hiyo alibainisha kuwa, mpango wa elimu kwa umma
umelenga kubadilisha fikra, mtazamo na imani potofu juu ya watu wenye
ualibinism. “Ni
dhahiri kuwa iwapo jamii itaelewa dhana nzima ya Ualbinism na kubadili
fikra na dhana potofu dhidi ya watu hawa, kuna uwezekani mkubwa wa
kukomesha kabisa matendo maouvu dhidi ya ndugu zetu wenye Ualbinism”
alieleza Kimishna Mandopi.

Mkuu
wa ofisi na mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi
na Utamaduni, Bi. Zulmira Rodrigues akizungumza kwa msisitizo juu ya
jamii ya watanzania kuchukua hatua ya kuwalinda watu wenye Ualbinism
nchini wakati wa tukio maalum la maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya
Uelimishaji Umma kuhusu Ualbino, iliyoandaliwa na tume ya Haki za
Binadamu na Utawala Bora nchini.
kushoto kwake ni Wakili wa Serikali na Mratibu wa masuala ya Albinism nchini, Bi Beatrice Mpangala. Kwa
upande wake Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa
la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Bi. Zulmira Rodrigues
alisisitiza jamii nchini kuongeza upendo pamoja na kuachana na imani
potofu inayosababisha kukithiri kwa vitendo hivyo hapa nchini.
No comments:
Post a Comment